< Zaburi 64 >
1 Sikia sauti yangu, Mungu, usikilize malalamiko yangu; unilinde dhidi ya hofu ya adui zangu.
To the chief music-maker. A Psalm. Of David. O God, let the voice of my grief come to your ear: keep my life from the fear of those who are against me.
2 Unifiche dhidi ya mipango ya siri ya wafanyao maovu, unifiche dhidi ya watendao vurugu ya udhalimu.
Keep me safe from the secret purpose of wrongdoers; from the band of the workers of evil;
3 Wao wamenoa ndimi zao kama panga; wamelenga mishale yao, maneno machungu,
Who make their tongues sharp like a sword, and whose arrows are pointed, even bitter words;
4 ili kwamba waweze kupiga kutoka mahali pa siri kwenda kwa mtu asiye na hatia; wampige yeye kwa ghafla nao wasihofu lolote.
So that in secret they may let loose their arrows at the upright, suddenly and unseen.
5 Wao wanahamasishana wenyewe katika kupanga uovu; wanashauriana pamoja wao binafsi ili kuweka mitego; nao husema, “Ni nani atakayetuona?”
They make themselves strong in an evil purpose; they make holes for secret nets; they say, Who will see it,
6 Wanabuni mipango ya dhambi; “Tumemaliza,” wanasema, “ni mpango makini.” Mawazo ya ndani na mioyo ya watu ni ya kina.
Or make discovery of our secret purpose? The design is framed with care; and the inner thought of a man, and his heart, is deep.
7 Lakini Mungu atawapiga wao; ghafla watajeruhiwa kwa mishale yake.
But God sends out an arrow against them; suddenly they are wounded.
8 Watafanywa kuwa mashakani, kwa kuwa ndimi zao wenyewe ziko kinyume nao; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao.
The evil of their tongues is the cause of their fall; all those who see them are shaking their heads at them.
9 Watu wote wataogopa na kutangaza matendo ya Mungu. Kwa hekima watafikiria kuhusu kile yeye ametenda.
And in fear men make public the works of God; and giving thought to his acts they get wisdom.
10 Wenye haki watakuwa na furaha kuhusu Yahwe nao watakimbilia kwake; wote wenye haki moyoni watajivuna katika yeye.
The upright will be glad in the Lord and have hope in him; and all the lovers of righteousness will give him glory.