< Zaburi 63 >
1 Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
Oh ʼElohim, Tú eres mi ʼEL. Ansiosamente te busqué. Mi alma tiene sed de Ti. Mi cuerpo te anhela en tierra árida y deshabitada, Donde no hay agua.
2 Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
Así te busqué en el Santuario Para ver tu poder y tu gloria.
3 Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
Porque tu misericordia es mejor que la vida, Mis labios te alabarán.
4 Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
Por tanto te bendeciré en mi vida. En tu Nombre alzaré mis manos.
5 Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
Como con médula y sustancia está saciada mi alma. Mi boca te alaba con labios jubilosos.
6 nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
Cuando en mi cama me acuerdo de Ti, Cuando medito en Ti en las vigilias de la noche.
7 Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
Porque Tú eres mi Socorro. Bajo la sombra de tus alas canto con gozo.
8 Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
Mi alma está apegada a Ti. Tu mano derecha me sostiene.
9 Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
Pero los que buscan mi vida para destruirla Caerán en las profundidades más bajas de la tierra.
10 watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
Serán destruidos a filo de espada. Serán presa de los chacales.
11 Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.
Pero el rey se regocija en ʼElohim. Cualquiera que jura por Él será alabado, Porque las bocas de los que dicen mentiras serán tapadas.