< Zaburi 63 >

1 Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
Un psaume de David, quand il était dans le désert de Judée. Dieu, tu es mon Dieu. Je vous chercherai sincèrement. Mon âme a soif de toi. Ma chair se languit de vous, dans une terre sèche et épuisée, où il n'y a pas d'eau.
2 Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
Je t'ai donc vu dans le sanctuaire, en regardant ta puissance et ta gloire.
3 Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
Parce que ta bonté est meilleure que la vie, mes lèvres te loueront.
4 Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
Je te bénirai donc tant que je vivrai. Je lèverai mes mains en ton nom.
5 Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
Mon âme sera rassasiée comme d'un mets riche. Ma bouche te louera avec des lèvres joyeuses,
6 nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
quand je me souviens de toi sur mon lit, et penser à toi dans les veilles de la nuit.
7 Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
Car c'est toi qui m'as aidé. Je me réjouirai à l'ombre de tes ailes.
8 Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
Mon âme reste près de toi. Ta main droite me soutient.
9 Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
Mais ceux qui cherchent mon âme pour la détruire iront dans les parties inférieures de la terre.
10 watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
Ils seront livrés à la puissance de l'épée. Ils seront de la nourriture pour chacals.
11 Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.
Mais le roi se réjouira en Dieu. Tous ceux qui jurent par lui le loueront, car la bouche de ceux qui disent des mensonges sera réduite au silence.

< Zaburi 63 >