< Zaburi 63 >
1 Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
A Psalm of David, when he was in the wilderness of Idumea. O God, my God, I cry to you early; my soul has thirsted for you: how often has my flesh [longed] after you, in a barren and trackless and dry land!
2 Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
Thus have I appeared before you in the sanctuary, that I might see your power and your glory.
3 Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
For your mercy is better than life: my lips shall praise you.
4 Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
Thus will I bless you during my life: I will lift up my hands in your name.
5 Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
Let my soul be filled as with marrow and fatness; and [my] joyful lips shall praise your name.
6 nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
Forasmuch as I have remembered you on my bed: in the early seasons I have meditated on you.
7 Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
For you have been my helper, and in the shelter of your wings will I rejoice.
8 Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
My soul has kept very close behind you: your right hand has upheld me.
9 Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
But they vainly sought after my soul; they shall go into the lowest parts o the earth.
10 watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
They shall be delivered up to the power of the sword; they shall be portions for foxes.
11 Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.
But the king shall rejoice in God; every one that swears by him shall be praised; for the mouth of them that speak unjust things has been stopped.