< Zaburi 63 >
1 Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
A psalm of David, when he was in the Judean desert. God, you are my God, I eagerly look for you. I am thirsty for you; all that I am longs for you in this dry, weary, waterless land.
2 Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
I see you in the Temple; I watch your power and glory.
3 Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
Your trustworthy love is better than life itself; I will praise you.
4 Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
I will thank you as long as I live; I lift up my hands as I celebrate your wonderful character.
5 Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
You satisfy me more than the richest food; I will praise you with joyful songs.
6 nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
I think of you all night long as I lie on my bed meditating about you.
7 Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
For you are the one who helps me; I sing happily from under your wings.
8 Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
I hold on to you; your strong arms lift me up.
9 Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
Those who are trying to destroy me will go down into the grave.
10 watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
They will be killed by the sword; they will become food for jackals.
11 Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.
But the king will be happy for what God has done. All who follow God will praise him, but those who tell lies will be silenced.