< Zaburi 63 >

1 Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
A Psalm of David, when he was in the desert of Idumea. O God, my God: to you, I keep vigil until first light. For you, my soul has thirsted, to you my body, in so many ways.
2 Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
By a deserted land, both inaccessible and waterless, so I have appeared in the sanctuary before you, in order to behold your virtue and your glory.
3 Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
For your mercy is better than life itself. It is you my lips will praise.
4 Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
So will I bless you in my life, and I will lift up my hands in your name.
5 Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
Let my soul be filled, as if with marrow and fatness; and my mouth will give praise with exultant lips.
6 nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
When I have remembered you on my bed in the morning, I will meditate on you.
7 Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
For you have been my helper. And I will exult under the cover of your wings.
8 Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
My soul has clung close to you. Your right hand has supported me.
9 Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
Truly, these ones have sought my soul in vain. They will enter into the lower parts of the earth.
10 watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
They will be delivered into the hand of the sword. They will be the portions of foxes.
11 Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.
Truly, the king will rejoice in God: all those who swear by him will be praised, because the mouth of those who speak iniquity has been blocked.

< Zaburi 63 >