< Zaburi 62 >

1 Katika ukimya ninamsubiri Mungu pekee; wokovu wangu watoka kwake.
in finem pro Idithun psalmus David nonne Deo subiecta erit anima mea ab ipso enim salutare meum
2 Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu; yeye ni mnara wangu mrefu; sitasogezwa kamwe.
nam et ipse Deus meus et salutaris meus susceptor meus non movebor amplius
3 Mpaka lini, ninyi nyote, mtamshambulia mtu, ili kwamba mumpindue yeye kama ukuta ulio inama au kama fensi isiyo imara?
quousque inruitis in hominem interficitis universi vos tamquam parieti inclinato et maceriae depulsae
4 Wanashauliana naye ili tu kumshusha chini kutoka kwenye nafasi yake heshimiwa; wao wanapenda kuongea uongo; wanambariki yeye kwa midomo yao, lakini mioyoni mwao wana mlaani yeye. (Selah)
verumtamen pretium meum cogitaverunt repellere cucurri in siti ore suo benedicebant et corde suo maledicebant diapsalma
5 Katika ukimya ninamsubiri Mungu pekee; kwa maana matumaini yangu yako kwake.
verumtamen Deo subiecta esto anima mea quoniam ab ipso patientia mea
6 Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu; yeye ni mnara wangu mrefu; sitasogezwa.
quia ipse Deus meus et salvator meus adiutor meus non emigrabo
7 Na Mungu ni wokovu wangu na utukufu wangu; mwamba wa nguvu yangu na kimbilio langu salama liko katika Mungu.
in Deo salutare meum et gloria mea Deus auxilii mei et spes mea in Deo est
8 Mwaminini Mungu wakati wote, ninyi watu; mimina moyo wako mbele zake; Mungu ni kimbilio salama kwa ajili yetu. (Selah)
sperate in eo omnis congregatio populi effundite coram illo corda vestra Deus adiutor noster in aeternum
9 Hakika watu wenye msimamo mdogo ni ubatili, na watu wenye msimamo mkubwa ni waongo; wao watakuwa wepesi kwenye mzani; uzito wao pamoja ni wepesi kuliko kitu chochote.
verumtamen vani filii hominum mendaces filii hominum in stateris ut decipiant ipsi de vanitate in id ipsum
10 Usiamini katika ukandamizaji au wizi; usitumainie utajiri, maana hawatazaa matunda; usiuweke moyo wako kwenye hivyo.
nolite sperare in iniquitate et rapinas nolite concupiscere divitiae si affluant nolite cor adponere
11 Mungu ameongea mara moja, mara mbili nimesikia hili: nguvu ni za Mungu.
semel locutus est Deus duo haec audivi quia potestas Dei
12 Pia kwako, Bwana, ni uaminifu wa agano, maana humlipa kila mtu kwa kile alichokifanya.
et tibi Domine misericordia quia tu reddes unicuique iuxta opera sua

< Zaburi 62 >