< Zaburi 62 >

1 Katika ukimya ninamsubiri Mungu pekee; wokovu wangu watoka kwake.
Au maître-chantre. — Selon Jéduthun. — Psaume de David. Mon âme se repose en paix sur Dieu seul; C'est de lui que vient mon salut.
2 Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu; yeye ni mnara wangu mrefu; sitasogezwa kamwe.
Seul il est mon rocher, mon salut, Ma haute retraite; je ne serai pas beaucoup ébranlé.
3 Mpaka lini, ninyi nyote, mtamshambulia mtu, ili kwamba mumpindue yeye kama ukuta ulio inama au kama fensi isiyo imara?
Jusques à quand vous jetterez-vous sur un homme. Pour l'abattre tous ensemble. Comme un mur qui penche. Comme une clôture qu'on renverse?
4 Wanashauliana naye ili tu kumshusha chini kutoka kwenye nafasi yake heshimiwa; wao wanapenda kuongea uongo; wanambariki yeye kwa midomo yao, lakini mioyoni mwao wana mlaani yeye. (Selah)
Ils ne pensent qu'à le faire tomber du poste où il s'est élevé; Ils se plaisent au mensonge. De leur bouche ils bénissent. Mais au fond du coeur ils maudissent. (Pause)
5 Katika ukimya ninamsubiri Mungu pekee; kwa maana matumaini yangu yako kwake.
Oui, sur Dieu seul mon âme se repose en paix; Car mon espoir est en lui.
6 Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu; yeye ni mnara wangu mrefu; sitasogezwa.
Seul, il est mon rocher, mon salut. Ma haute retraite: je ne serai point ébranlé!
7 Na Mungu ni wokovu wangu na utukufu wangu; mwamba wa nguvu yangu na kimbilio langu salama liko katika Mungu.
C'est de Dieu que j'attends mon salut et ma gloire: Dieu est mon rocher protecteur; mon refuge est en lui.
8 Mwaminini Mungu wakati wote, ninyi watu; mimina moyo wako mbele zake; Mungu ni kimbilio salama kwa ajili yetu. (Selah)
Peuples, confiez-vous en lui en tout temps! Répandez devant lui votre coeur: Dieu est notre refuge! (Pause)
9 Hakika watu wenye msimamo mdogo ni ubatili, na watu wenye msimamo mkubwa ni waongo; wao watakuwa wepesi kwenye mzani; uzito wao pamoja ni wepesi kuliko kitu chochote.
Les petits ne sont que néant; Les grands ne sont que mensonge: Placés dans la balance, Ils pèseraient tous ensemble moins que le néant même.
10 Usiamini katika ukandamizaji au wizi; usitumainie utajiri, maana hawatazaa matunda; usiuweke moyo wako kwenye hivyo.
Ne mettez pas votre confiance dans la violence; Ne mettez pas un vain espoir dans la rapine. Si vos richesses abondent, N'y attachez pas votre coeur!
11 Mungu ameongea mara moja, mara mbili nimesikia hili: nguvu ni za Mungu.
Dieu a dit une fois. Et j'ai entendu sa voix redire encore: «La force appartient à Dieu!»
12 Pia kwako, Bwana, ni uaminifu wa agano, maana humlipa kila mtu kwa kile alichokifanya.
A toi aussi, Seigneur, la miséricorde! Tu rendras à chacun selon ses oeuvres.

< Zaburi 62 >