< Zaburi 62 >

1 Katika ukimya ninamsubiri Mungu pekee; wokovu wangu watoka kwake.
Pour le chef musicien. A Jeduthun. Un psaume de David. Mon âme repose en Dieu seul. Mon salut vient de lui.
2 Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu; yeye ni mnara wangu mrefu; sitasogezwa kamwe.
Lui seul est mon rocher, mon salut et ma forteresse. Je ne serai jamais fortement ébranlé.
3 Mpaka lini, ninyi nyote, mtamshambulia mtu, ili kwamba mumpindue yeye kama ukuta ulio inama au kama fensi isiyo imara?
Combien de temps allez-vous agresser un homme? Vous voulez tous le jeter à terre, comme un mur penché, comme une clôture chancelante?
4 Wanashauliana naye ili tu kumshusha chini kutoka kwenye nafasi yake heshimiwa; wao wanapenda kuongea uongo; wanambariki yeye kwa midomo yao, lakini mioyoni mwao wana mlaani yeye. (Selah)
Ils ont bien l'intention de le jeter à bas de sa position élevée. Ils se délectent de mensonges. Ils bénissent de la bouche, mais ils maudissent intérieurement. (Selah)
5 Katika ukimya ninamsubiri Mungu pekee; kwa maana matumaini yangu yako kwake.
Mon âme, attends en silence Dieu seul, car c'est de lui que je m'attends.
6 Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu; yeye ni mnara wangu mrefu; sitasogezwa.
Lui seul est mon rocher, mon salut, ma forteresse. Je ne serai pas ébranlé.
7 Na Mungu ni wokovu wangu na utukufu wangu; mwamba wa nguvu yangu na kimbilio langu salama liko katika Mungu.
Mon salut et mon honneur sont auprès de Dieu. Le rocher de ma force, et mon refuge, est en Dieu.
8 Mwaminini Mungu wakati wote, ninyi watu; mimina moyo wako mbele zake; Mungu ni kimbilio salama kwa ajili yetu. (Selah)
Ayez confiance en lui en tout temps, vous autres. Répandez votre cœur devant lui. Dieu est un refuge pour nous. (Selah)
9 Hakika watu wenye msimamo mdogo ni ubatili, na watu wenye msimamo mkubwa ni waongo; wao watakuwa wepesi kwenye mzani; uzito wao pamoja ni wepesi kuliko kitu chochote.
Les hommes de peu de valeur ne sont qu'un souffle, et les hommes de haut rang sont un mensonge. Dans les soldes, ils vont augmenter. Ils sont ensemble plus légers qu'un souffle.
10 Usiamini katika ukandamizaji au wizi; usitumainie utajiri, maana hawatazaa matunda; usiuweke moyo wako kwenye hivyo.
Ne vous fiez pas à l'oppression. Ne devenez pas vaniteux dans le vol. Si les richesses augmentent, n'y attachez pas votre cœur.
11 Mungu ameongea mara moja, mara mbili nimesikia hili: nguvu ni za Mungu.
Dieu a parlé une fois; J'ai entendu cela deux fois, ce pouvoir appartient à Dieu.
12 Pia kwako, Bwana, ni uaminifu wa agano, maana humlipa kila mtu kwa kile alichokifanya.
A toi aussi, Seigneur, appartient la bonté, car tu récompenses chaque homme selon son travail.

< Zaburi 62 >