< Zaburi 62 >
1 Katika ukimya ninamsubiri Mungu pekee; wokovu wangu watoka kwake.
To the Chief Musician. On Jeduthun—A Melody of David. Surely, towards God, silence [becometh] my soul, From him, is my salvation:
2 Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu; yeye ni mnara wangu mrefu; sitasogezwa kamwe.
Surely, he, is my rock and my salvation, My high tower—I shall not be greatly shaken!
3 Mpaka lini, ninyi nyote, mtamshambulia mtu, ili kwamba mumpindue yeye kama ukuta ulio inama au kama fensi isiyo imara?
How long will ye shout at a man? Ye shall be crushed all of you, —Like a wall that bulgeth, —a fence pushed in!
4 Wanashauliana naye ili tu kumshusha chini kutoka kwenye nafasi yake heshimiwa; wao wanapenda kuongea uongo; wanambariki yeye kwa midomo yao, lakini mioyoni mwao wana mlaani yeye. (Selah)
Surely, from his elevation, they have taken counsel to thrust him down, They accept falsehood, —With his mouth, they each of them bless, But, inwardly, they revile. (Selah)
5 Katika ukimya ninamsubiri Mungu pekee; kwa maana matumaini yangu yako kwake.
Surely, towards God, be thou silent, my soul, For, from him, is mine expectation:
6 Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu; yeye ni mnara wangu mrefu; sitasogezwa.
Surely, he, is my rock, and my salvation, My high tower—I shall not be shaken!
7 Na Mungu ni wokovu wangu na utukufu wangu; mwamba wa nguvu yangu na kimbilio langu salama liko katika Mungu.
Upon God, [depend] my salvation and mine honour, My rock of strength, my refuge, are in God.
8 Mwaminini Mungu wakati wote, ninyi watu; mimina moyo wako mbele zake; Mungu ni kimbilio salama kwa ajili yetu. (Selah)
Trust ye in him all ye assembly of the people, Pour out, before him, your heart, God, is a refuge for us. (Selah)
9 Hakika watu wenye msimamo mdogo ni ubatili, na watu wenye msimamo mkubwa ni waongo; wao watakuwa wepesi kwenye mzani; uzito wao pamoja ni wepesi kuliko kitu chochote.
Surely, vanity, are men of low degree, Deception, men of high degree, —In the balances, they go up, They, are [made] of vanity, altogether.
10 Usiamini katika ukandamizaji au wizi; usitumainie utajiri, maana hawatazaa matunda; usiuweke moyo wako kwenye hivyo.
Do not trust in extortion, Nor, with robbery, become vain, As for wealth, when it beareth fruit, Do not set [thereon your] heart.
11 Mungu ameongea mara moja, mara mbili nimesikia hili: nguvu ni za Mungu.
One thing, hath God spoken, Two things, [there are] which I have heard, That, power, belongeth unto God;
12 Pia kwako, Bwana, ni uaminifu wa agano, maana humlipa kila mtu kwa kile alichokifanya.
And, thine, O My Lord, is lovingkindness, —For, thou, wilt pay back unto every man—according to his deed.