< Zaburi 62 >
1 Katika ukimya ninamsubiri Mungu pekee; wokovu wangu watoka kwake.
For Jeduthun, the music director. A psalm of David. Only in God do I find peace; my salvation comes from him.
2 Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu; yeye ni mnara wangu mrefu; sitasogezwa kamwe.
He is the one who protects me and saves me; he keeps me safe so I will never be in danger.
3 Mpaka lini, ninyi nyote, mtamshambulia mtu, ili kwamba mumpindue yeye kama ukuta ulio inama au kama fensi isiyo imara?
How long are you going to attack me? All of you against one man! To you I'm just a broken wall, a collapsed fence.
4 Wanashauliana naye ili tu kumshusha chini kutoka kwenye nafasi yake heshimiwa; wao wanapenda kuongea uongo; wanambariki yeye kwa midomo yao, lakini mioyoni mwao wana mlaani yeye. (Selah)
They plan to throw me down from my high position; they love to tell lies. They say nice things to me, but inside they're cursing me. (Selah)
5 Katika ukimya ninamsubiri Mungu pekee; kwa maana matumaini yangu yako kwake.
Only in God do I find peace; my hope comes from him.
6 Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu; yeye ni mnara wangu mrefu; sitasogezwa.
He is the one who protects me and saves me; he keeps me safe so I will not be in danger.
7 Na Mungu ni wokovu wangu na utukufu wangu; mwamba wa nguvu yangu na kimbilio langu salama liko katika Mungu.
My salvation and my success come from God alone; God is my security and my protection.
8 Mwaminini Mungu wakati wote, ninyi watu; mimina moyo wako mbele zake; Mungu ni kimbilio salama kwa ajili yetu. (Selah)
My people, always trust in him. Pour out all your thoughts to him, for he is the one who looks after us. (Selah)
9 Hakika watu wenye msimamo mdogo ni ubatili, na watu wenye msimamo mkubwa ni waongo; wao watakuwa wepesi kwenye mzani; uzito wao pamoja ni wepesi kuliko kitu chochote.
Ordinary people are mere breaths, while leaders are just fakes. Put them all together and weigh them on scales and they wouldn't weigh more than air!
10 Usiamini katika ukandamizaji au wizi; usitumainie utajiri, maana hawatazaa matunda; usiuweke moyo wako kwenye hivyo.
Don't trust in money made by extortion or robbery. Don't be proud of your wealth even if you are successful—don't make money what you live for.
11 Mungu ameongea mara moja, mara mbili nimesikia hili: nguvu ni za Mungu.
God has already made it clear—I have heard it many times—power belongs to you, God.
12 Pia kwako, Bwana, ni uaminifu wa agano, maana humlipa kila mtu kwa kile alichokifanya.
You show us trustworthy love. You give back to people in return for what they've done.