< Zaburi 62 >

1 Katika ukimya ninamsubiri Mungu pekee; wokovu wangu watoka kwake.
My soul waits in silence for God only. From him is my salvation.
2 Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu; yeye ni mnara wangu mrefu; sitasogezwa kamwe.
He only is my rock and my salvation, my high tower. I shall not be greatly moved.
3 Mpaka lini, ninyi nyote, mtamshambulia mtu, ili kwamba mumpindue yeye kama ukuta ulio inama au kama fensi isiyo imara?
How long will ye set upon a man, that ye may kill, all of you, like a leaning wall, like a tottering fence?
4 Wanashauliana naye ili tu kumshusha chini kutoka kwenye nafasi yake heshimiwa; wao wanapenda kuongea uongo; wanambariki yeye kwa midomo yao, lakini mioyoni mwao wana mlaani yeye. (Selah)
They only consult to thrust him down from his dignity. They delight in lies. They bless with their mouth, but they curse inwardly. (Selah)
5 Katika ukimya ninamsubiri Mungu pekee; kwa maana matumaini yangu yako kwake.
My soul, wait thou in silence for God only, for my expectation is from him.
6 Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu; yeye ni mnara wangu mrefu; sitasogezwa.
He only is my rock and my salvation, my high tower. I shall not be moved.
7 Na Mungu ni wokovu wangu na utukufu wangu; mwamba wa nguvu yangu na kimbilio langu salama liko katika Mungu.
With God is my salvation and my glory. The rock of my strength, and my refuge, is in God.
8 Mwaminini Mungu wakati wote, ninyi watu; mimina moyo wako mbele zake; Mungu ni kimbilio salama kwa ajili yetu. (Selah)
Trust in him at all times, ye people. Pour out your heart before him. God is a refuge for us. (Selah)
9 Hakika watu wenye msimamo mdogo ni ubatili, na watu wenye msimamo mkubwa ni waongo; wao watakuwa wepesi kwenye mzani; uzito wao pamoja ni wepesi kuliko kitu chochote.
Surely men of low degree are vanity, and men of high degree are a lie. In the balances they will go up. They are together lighter than vanity.
10 Usiamini katika ukandamizaji au wizi; usitumainie utajiri, maana hawatazaa matunda; usiuweke moyo wako kwenye hivyo.
Trust not in oppression, and become not vain in robbery. If riches increase, set not your heart on it.
11 Mungu ameongea mara moja, mara mbili nimesikia hili: nguvu ni za Mungu.
God has spoken once, twice I have heard this, that power belongs to God.
12 Pia kwako, Bwana, ni uaminifu wa agano, maana humlipa kila mtu kwa kile alichokifanya.
Also to thee, O Lord, belongs loving kindness, for thou render to every man according to his work.

< Zaburi 62 >