< Zaburi 60 >
1 Mungu, wewe umetutupa; umeuvunja ulinzi wetu; wewe umekuwa hasirani; utuwezeshe tena.
To the chief Musician upon Shushaneduth, Michtam of David, to teach; when he strove with Aramnaharaim and with Aramzobah, when Joab returned, and smote of Edom in the valley of salt twelve thousand. O God, thou hast cast us off, thou hast scattered us, thou hast been displeased; O turn thyself to us again.
2 Wewe umeifanya nchi kutetemeka; umeipasua pasua; uiponye nyufa zake, maana zinatikisika.
Thou hast made the earth to tremble; thou hast broken it: heal its breaches; for it shaketh.
3 Wewe umewafanya watu wako kuona mambo magumu; umetufanya tunywe mvinyo wenye kutufanya kupepesuka.
Thou hast shown thy people hard things: thou hast made us to drink the wine of astonishment.
4 Kwa wale wanao kuheshimu wewe, wewe umeweka bandera ionekane dhidi ya wale wabebao upinde. (Selah)
Thou hast given a banner to them that fear thee, that it may be displayed because of the truth. (Selah)
5 Ili kwamba wale uwapendao waweze kuokolewa, utuokoe sisi kwa mkono wako wa kuume na unijibu.
That thy beloved may be delivered; save with thy right hand, and hear me.
6 Mungu ameongea katika utakatifu wake, “Nitashangilia; nitaigawanya Shekemu na kuligawa bonde la Sukothi.
God hath spoken in his holiness; I will rejoice, I will divide Shechem, and measure out the valley of Succoth.
7 Gileadi ni yangu, na Manase ni yangu na Ephraimu pia ni kofia yangu ya chuma; Yuda ni fimbo yangu ya kifalme.
Gilead is mine, and Manasseh is mine; Ephraim also is the strength of my head; Judah is my lawgiver;
8 Moabu ni bakuli langu la kunawia; juu ya Edomu nitatupa kiatu changu; nitapiga kelele za ushindi kwa sababu ya Filisti.”
Moab is my washpot; over Edom will I cast out my shoe: Philistia, triumph thou because of me.
9 Ni nani atakaye nileta kwenye mji imara? Ni nani ataniongoza kwenda Edomu?
Who will bring me into the strong city? who will lead me into Edom?
10 Lakini wewe, Mungu, je, haukutukataa? Wewe hauendi vitani pamoja na jeshi letu.
Wilt thou not, O God, who hadst cast us off? and thou, O God, who didst not go out with our armies?
11 Utusaidie dhidi ya adui yetu, maana msaada wa mwanadamu ni bure.
Give us help from trouble: for vain is the help of man.
12 Kwa msaada wa Mungu tutashinda; yeye atawakanyaga chini adui zetu.
Through God we shall do valiantly: for he will tread down our enemies.