< Zaburi 6 >

1 Yahweh, usinikemee ukiwa na hasira au usiniadhibu katika gadhabu yako.
For the leader; with instrumental music on the sheminith. A psalm of David. Rebuke me not, Lord, in your anger, punish me not in your wrath.
2 Unihurumie, Yahwe, kwa maana ni dhaifu; uniponye, Yahweh, kwa kuwa mifupa yangu ina tikisika.
Lord, be gracious to me in my weakness. Heal me Lord, for racked is my body;
3 Moyo wangu pia umesumbuka sana. Lakini wewe, Yahweh, mpaka lini hali hii itaendelea?
all of me utterly racked. Why do you wait so long, Lord?
4 Rudi, Yahweh! uniokoe. Uniokoe kwa sababu ya uaminifu wa agano lako!
Turn, Lord, rescue me; save me, because of your love.
5 kwa kuwa kifoni hakuna kumbukumbu lako. Kuzimuni ni nani atakaye kushukuru? (Sheol h7585)
For in death none can call you to mind; in Sheol who can praise you? (Sheol h7585)
6 Nimechoshwa na kuugua kwangu. Ninalowanisha kitanda changu kwa machozi usiku kucha; ninaosha kiti changu kwa machozi.
I am so weary of sighing. All the night I make my bed swim, and wet my couch with my tears.
7 Macho yangu yanafifia kwa kulia sana; yanazidi kuwa dhaifu kwa sababu ya adaui zangu.
My eyes swollen with grief; from weeping caused by my foes.
8 Ondokeni kwangu, nyote mtendao maovu; kwa kuwa Yahweh amesikia sauti ya kilio changu.
Begone, workers of wrong, for the Lord has heard my loud weeping,
9 Yahweh amesikia malalamiko yangu kwa ajili ya huruma; Yahweh ameyapokea maombi yangu.
the Lord has heard my entreaty, the Lord accepts my prayer.
10 Maadui zangu wote wataaibishwa na kuteswa sana. Watarudi nyuma na ghafra kufedheheshwa.
My foes will be stricken with terror, brought to shame and dismay in a moment.

< Zaburi 6 >