< Zaburi 59 >
1 Uniokoe dhidi ya adui zangu, Mungu wangu; uniweke mahali pa juu mbali na wale wanaoinuka dhidi yangu.
To him that excelleth. Destroy not. A Psalme of David on Michtam. When Saul sent and they did watch the house to kill him. O my God, deliuer mee from mine enemies: defend me from them that rise vp against me.
2 Uniweke salama mbali na wafanyao kazi ya uovu, na uniokoe dhidi ya watu wenye kiu ya damu.
Deliuer me from the wicked doers, and saue me from the bloody men.
3 Maana, tazama, wanasubiria uvamizini waniue. Wafanya maovu wenye nguvu hujikusanya wenyewe pamoja dhidi yangu, lakini sio kwa sababu ya makosa yangu au dhambi yangu, Yahwe.
For loe, they haue layd waite for my soule: the mightie men are gathered against me, not for mine offence, nor for my sinne, O Lord.
4 Wao wanajiandaa kunikimbiza ingawa sina kosa; amka unisaidie na unitazame.
They runne and prepare themselues without a fault on my part: arise therefore to assist me, and beholde.
5 Ewe, Yahwe Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, inika uwaadhibu mataifa yote; usiwe na huruma kwa mhalifu mwovu yeyote. (Selah)
Euen thou, O Lord God of hostes, O God of Israel awake to visit all the heathen, and be not merciful vnto all that transgresse maliciously. (Selah)
6 Wao wanarudi jioni, wanabweka kama mbwa na kuuzungukia mji.
They goe to and from in the euening: they barke like dogs, and goe about the citie.
7 Tazama, wanapiga kelele mbaya kwa midomo yao; panga ziko kwenye midomo yao, maana wanasema, “Ni nani anaye tusikia?”
Behold, they brag in their talke, and swords are in their lips: for, Who, say they, doeth heare?
8 Lakini wewe, Yahwe, utawacheka; wewe huwadhihaki mataifa yote.
But thou, O Lord, shalt haue them in derision, and thou shalt laugh at all the heathen.
9 Mungu, nguvu yangu, nitakuwa msikivu kwako; wewe ni mnara wangu mrefu.
He is strong: but I will waite vpon thee: for God is my defence.
10 Mungu atakutana nami akiwa na uaminifu wa agano lake; Mungu atanifanya nione shauku yangu juu ya adui zangu.
My mercifull God will preuent me: God wil let me see my desire vpon mine enemies.
11 Usiwaue, hivyo watu watasahau. Uwatawanye kwa nguvu zako na uwaangushe, Bwana ngao yetu.
Slay them not, least my people forget it: but scatter them abroad by thy power, and put them downe, O Lord our shield,
12 Kwa ajili ya dhambi za midomo yao na maneno ya midomo yao, wakamatwe katika majivuno yao, na kwa laana na uongo ambao wao huelezea.
For the sinne of their mouth, and the words of their lips: and let them be taken in their pride, euen for their periurie and lies, that they speake.
13 Uwamalize katika gadhabu yako, uwamalize ili kwamba wasiwepo tena; wajue kuwa Mungu anatawala katika Yakobo na mwisho wa nchi. (Selah)
Consume them in thy wrath: consume them that they be no more: and let them knowe that God ruleth in Iaakob, euen vnto the ends of the world. (Selah)
14 Wakati wa jioni wao hurudi, wakibweka kama mbwa wakiuzungukia mji.
And in the euening they shall go to and from, and barke like dogs, and go about the citie.
15 Wanatangatanga wakitafuta chakula na wanabweka kama mbwa kama hawajatosheka.
They shall runne here and there for meate: and surely they shall not be satisfied, though they tary all night.
16 Lakini nitaimba kuhusu nguvu zako, na asubuhi nitaimba kuhusu upendo wako imara! maana umekuwa mnara wangu mrefu na kimbilio la usalama katika siku ya taabu.
But I wil sing of thy power, and will prayse thy mercy in the morning: for thou hast bene my defence and refuge in the day of my trouble.
17 Kwako, nguvu yangu, nitaimba sifa; kwa kuwa Mungu ni mnara wangu mrefu, Mungu wa uaminifu wa agano.
Vnto thee, O my Strength, wil I sing: for God is my defence, and my mercifull God.