< Zaburi 57 >

1 Unihurumie, Mungu, unihurumie mimi, kwa maana ninakukimbilia wewe mpaka matatizo haya yaishe. Ninakaa chini ya mbawa za zako kwa ajili ya ulinzi mpaka huu uharibifu utakapoisha.
למנצח אל תשחת לדוד מכתם בברחו מפני שאול במערה חנני אלהים חנני כי בך חסיה נפשי ובצל כנפיך אחסה עד יעבר הוות׃
2 Nitakulilia Mungu uliye hai, kwa Mungu, afanyaye mambo yote kwa ajili yangu.
אקרא לאלהים עליון לאל גמר עלי׃
3 Yeye atatuma msaada kutoka mbinguni na kuniokoa, ana hasira na wale wanaonishambulia. (Selah) Mungu atanitumia upendo wake mwema na uaminifu wake.
ישלח משמים ויושיעני חרף שאפי סלה ישלח אלהים חסדו ואמתו׃
4 Uhai wangu uko katikati ya simba; niko katikati ya wale walio tayari kunila. Niko katikati ya watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, na ambao ndimi zao ni kali kama upanga.
נפשי בתוך לבאם אשכבה להטים בני אדם שניהם חנית וחצים ולשונם חרב חדה׃
5 Uinuliwe, Mungu, juu ya mbingu, utukufu wako uwe juu ya nchi yote.
רומה על השמים אלהים על כל הארץ כבודך׃
6 Wao walisambaza nje wavu kwa ajili ya miguu yangu; nilikuwa na shida sana. Walichimba shimo mbele yangu. Wao wenyewe wameangukia katikati ya shimo! (Selah)
רשת הכינו לפעמי כפף נפשי כרו לפני שיחה נפלו בתוכה סלה׃
7 Moyo wangu umeponywa, Mungu, moyo wangu umeponywa, nitaimba, ndiyo, nitaimba sifa.
נכון לבי אלהים נכון לבי אשירה ואזמרה׃
8 Inuka, moyo wa thamani; inuka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
עורה כבודי עורה הנבל וכנור אעירה שחר׃
9 Nitakushukuru wewe, Bwana, kati ya watu; Kati ya mataifa nitakuimbia sifa.
אודך בעמים אדני אזמרך בל אמים׃
10 Maana upendo wako usiokwisha, huzifikia mbingu; na uaminifu wako mawinguni.
כי גדל עד שמים חסדך ועד שחקים אמתך׃
11 Uinuliwe, Mungu, juu ya mbingu; na utukufu wako uinuliwe juu ya nchi yote.
רומה על שמים אלהים על כל הארץ כבודך׃

< Zaburi 57 >