< Zaburi 56 >

1 Uwe na huruma nami, Mungu, kwa maana watu wananishambulia! Muda wote wale wanao pigana nami hunikaribia zaidi ili wanishambulie.
Ten misericordia de mí, o! Dios; porque me traga el hombre; cada día batallándome aprieta.
2 Adui zangu hunikanyaga muda wote; maana ni wengi ambao kwa kiburi hupigana dhidi yangu.
Tráganme mis enemigos cada día: porque muchos son los que pelean contra mí, o! Altísimo.
3 Wakati nina woga, nitaweka imani yangu katika wewe.
De día temo: mas yo en ti confío.
4 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu - nimeweka imani yangu katika Mungu; sitaogopa; mtu wa kawaida atanifanya nini?
En Dios alabaré su palabra: en Dios he confiado, no temeré lo que la carne me hará.
5 Muda wote wanayageuza maneno yangu; mawazo yao yote yako kinyume na mimi kwa ajili ya uovu.
Todos los días me contristan mis negocios: contra mí son todos sus pensamientos para mal.
6 Wanajikusanya kwa pamoja, wanajificha wenyewe, na kuzifuatilia hatua zangu, wakisubiri kuniua.
Congréganse, escóndense, ellos miran atentamente mis pisadas esperando mi alma.
7 Usiwaache waikimbie adhabu yako kwa ajili ya uovu wao. Uwaangushe watu chini katika hasira yako, Mungu.
¿Por la iniquidad escaparán ellos? o! Dios, derriba los pueblos con furor.
8 Wewe unahesabu kutangatanga kwangu na kuweka machozi yangu kwenye chupa yako; je, hayako kitabuni mwako?
Mis huidas has contado tú; pon mis lágrimas en tu odre, ciertamente en tu libro.
9 Ndipo maadui zangu watakimbia katika siku ile nikuitapo wewe; hili najua, kwamba Mungu yupo kwa ajili yangu.
Entonces serán vueltos atrás mis enemigos el día que yo clamare: en esto conozco que Dios es por mí.
10 Katika Mungu ambaye neno lake ninalisifu, katika Yahwe ambaye neno lake ninalisifu,
En Dios alabaré su palabra; en Jehová alabaré su palabra.
11 katika Mungu ninaamini, sitaogopa. Yeyote atanifanya nini?
En Dios he confiado, no temeré lo que el hombre me hará.
12 Wajibu wa kutimiza viapo vyangu kwako uko juu yangu, Mungu; nitatoa sadaka ya shukurani.
Sobre mí, o! Dios, están tus votos: alabanzas te pagaré.
13 Kwa kuwa umeokoa uhai wangu na mauti; umezuia miguu yangu isianguke, ili kwamba niweze kutembea mbele ya Mungu katika nuru ya uhai.
Por cuanto has escapado mi vida de la muerte, ciertamente mis pies de caída: para que ande delante de Dios en la luz de los que viven.

< Zaburi 56 >