< Zaburi 56 >
1 Uwe na huruma nami, Mungu, kwa maana watu wananishambulia! Muda wote wale wanao pigana nami hunikaribia zaidi ili wanishambulie.
Au chef de musique. Sur Jonath-Élem-Rekhokim. De David. Mictam; quand les Philistins le prirent dans Gath. Use de grâce envers moi, ô Dieu! car l’homme voudrait m’engloutir; me faisant la guerre tout le jour, il m’opprime.
2 Adui zangu hunikanyaga muda wote; maana ni wengi ambao kwa kiburi hupigana dhidi yangu.
Mes ennemis voudraient tout le jour m’engloutir; car il y en a beaucoup qui me font la guerre, avec hauteur.
3 Wakati nina woga, nitaweka imani yangu katika wewe.
Au jour où je craindrai, je me confierai en toi.
4 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu - nimeweka imani yangu katika Mungu; sitaogopa; mtu wa kawaida atanifanya nini?
En Dieu, je louerai sa parole; en Dieu je me confie: je ne craindrai pas; que me fera la chair?
5 Muda wote wanayageuza maneno yangu; mawazo yao yote yako kinyume na mimi kwa ajili ya uovu.
Tout le jour ils tordent mes paroles; toutes leurs pensées sont contre moi en mal.
6 Wanajikusanya kwa pamoja, wanajificha wenyewe, na kuzifuatilia hatua zangu, wakisubiri kuniua.
Ils s’assemblent, ils se cachent, ils observent mes pas, car ils guettent mon âme.
7 Usiwaache waikimbie adhabu yako kwa ajili ya uovu wao. Uwaangushe watu chini katika hasira yako, Mungu.
Échapperont-ils par l’iniquité? Dans ta colère, ô Dieu, précipite les peuples!
8 Wewe unahesabu kutangatanga kwangu na kuweka machozi yangu kwenye chupa yako; je, hayako kitabuni mwako?
Tu comptes mes allées et mes venues; mets mes larmes dans tes vaisseaux; ne sont-elles pas dans ton livre?
9 Ndipo maadui zangu watakimbia katika siku ile nikuitapo wewe; hili najua, kwamba Mungu yupo kwa ajili yangu.
Alors mes ennemis retourneront en arrière, au jour où je crierai; je sais cela, car Dieu est pour moi.
10 Katika Mungu ambaye neno lake ninalisifu, katika Yahwe ambaye neno lake ninalisifu,
En Dieu, je louerai sa parole; en l’Éternel, je louerai sa parole.
11 katika Mungu ninaamini, sitaogopa. Yeyote atanifanya nini?
En Dieu je me confie: je ne craindrai pas; que me fera l’homme?
12 Wajibu wa kutimiza viapo vyangu kwako uko juu yangu, Mungu; nitatoa sadaka ya shukurani.
Les vœux que je t’ai faits sont sur moi, ô Dieu! je te rendrai des louanges.
13 Kwa kuwa umeokoa uhai wangu na mauti; umezuia miguu yangu isianguke, ili kwamba niweze kutembea mbele ya Mungu katika nuru ya uhai.
Car tu as délivré mon âme de la mort: [ne garderais-tu] pas mes pieds de broncher, pour que je marche devant Dieu dans la lumière des vivants?