< Zaburi 55 >
1 Uyategee sikio maombi yangu, Mungu; nawe usijifiche mbali na kusihi kwangu.
達味訓誨歌,交與槳官。 天主,求你側耳傾聽我的祈禱,求你不要迴避我的哀告。
2 Unitazame kwa makini na unijibu; Sina pumziko katika shida zangu
求你俯視我,並垂允我,我痛苦憂傷,嘆息悲號:
3 kwa sababu ya sauti ya adui zangu, kwa sababu ya ukandamizaji wa waovu; maana wananiletea matatizo na kunitesa wakiwa na hasira.
由於仇敵的叫囂,並因惡人的吵鬧,因加於我的災禍,怒中給我的騷擾,
4 Moyo wangu wasumbuka ndani yangu, na hofu ya kifo imeniangukia.
我的心在我胸內焦灼,死亡的恐怖籠罩了我,
5 Uwoga na kutetemeka kumenijia, nayo hofu imenielemea.
驚懼與戰慄侵襲了我,恐怖與煩惱淹沒了我。
6 Nikasema, “Oh, kama tu ningekuwa na mabawa kama njiwa! Ningelipaa mbali na kupata pumziko.
我於是說:但願我有鴿子般的翅膀,為能飛翔而去,棲身安藏!
7 Tazama, ningeenda mbali; ningekaa jangwani. (Selah)
看,我必要逃往遠處,在荒涼的地方暫住;
8 Ningefanya haraka kuja mafichoni mwako kuzikimbia dhoruba na tufani.”
從速尋找一個避難所,避過這一場風狂雨暴。
9 Uwaangamize, Bwana, vuruga lugha zao! Kwa maana nimeona vurugu na ugomvi katika mji.
我主,求你分散擾亂他們的語言,因我在城中只見到鬥爭與紛亂:
10 Mchana na usiku wao huenda kwenye kuta zake; uchafu na ufisadi uko katikati yake.
他們日夜在城牆上巡行,邪惡與欺壓在城中叢生。
11 Uovu uko katikati yake; ukandamizaji na uongo hauiachi mitaa yake.
城池中已滿布詭計,霸道欺詐橫行街市。
12 Kwa maana hakuwa adui aliye nikemea, hivyo ningevumilia; wala ingekuwa ni yule aliye nichukia aliyejiinua mwenyewe dhidi yagu, hivyo ningejificha asinione.
若是我的仇人辱罵我,我還可容忍;若是惱恨我者欺凌我,我尚可退隱;
13 Lakini ulikuwa wewe, mtu sawa na mimi, mwenzangu na rafiki yangu.
可惜是你,我的同僚,我的伙伴,我的友好;
14 Tulikuwa na ushirika mtamu pamoja; tuliingia katika nyumba ya Mungu tukiwa na umati mkubwa.
我們曾經推心置腹,無所諱言,在人群中走進了天主的聖殿。
15 Kifo na kiwapate ghafla; na washuke wakiwa hai kuzimuni, maana ndiko waishiko waovu, hapo hapo kati yao. (Sheol )
願死亡突襲他們,活活的墜入陰府!因為他們的居處和內心滿是惡毒。 (Sheol )
16 Lakini kwangu mimi, nitamwita Mungu, na Yahwe ataniokoa.
但我卻要呼號天主,上主必定予我救助。
17 Wakati wa jioni, asubuhi na mchana ninalalamika na kuomboleza; yeye atasikia sauti yangu.
不論在黃昏在清晨或在中午,我哀聲悲嘆,祂必聽我的苦訴。
18 Kwa usalama kabisa atayaokoa maisha yangu na vita dhidi yangu, kwa maana wale waliopigana nami walikuwa ni wengi.
祂必從迫害我的人中,救我然脫險,因為那些反對我的人,實在眾多難算。
19 Mungu, yule unayetawala milele, atawasikia na kuwaaibisha wao. (Selah) Hawabadiliki, na hawamhofu Mungu.
永遠為王的天主必要俯聽我,而把他們趕走,因為他們不知回心轉意,又不知敬愛天主。
20 Rafiki yangu ameinua mikono yake dhidi ya wale waliokuwa na amani naye; Hakuheshimu agano alilokuwa nalo.
他們伸手攻擊自己的友好,他們任意訂立違背的盟約。
21 Mdomo wake ulikuwa laini kama siagi, lakini moyo wake ulikuwa adui; maneno yake yalikuwa laini kuliko mafuta, lakini yalikuwa ni panga zilizochomolewa.
他們的容貌比奶油更光滑,心卻是好戰;他們的言語比脂粉還柔和,但口蜜腹劍。
22 Umtwike mizigo yako Yahwe, naye atakusaidia; yeye hataruhusu mtu mwenye haki kuyumbayumba.
將你的重擔卸交上主,祂必扶持你,祂決對不會讓義人永遠動搖不止。
23 Bali wewe, Mungu, utawaleta waovu chini kwenye shimo la uharibifu; watu wenye kiu ya kumwaga damu na waongo hawataishi hata nusu ya maisha kama wengine, lakini mimi nitakuamini wewe.
天主,求你使他們墮入滅亡的深穴!兇手和奸詐的歹徒必定中年夭折。上主,但我卻要時常一心唯你是賴。