< Zaburi 54 >

1 Uniokoe, Mungu, kwa jina lako, na kwa nguvu zako unihukumu.
למנצח בנגינת משכיל לדוד בבוא הזיפים ויאמרו לשאול הלא דוד מסתתר עמנו אלהים בשמך הושיעני ובגבורתך תדינני׃
2 Usikie maombi yangu, Mungu; uyategee sikio maneno ya mdomo wangu.
אלהים שמע תפלתי האזינה לאמרי פי׃
3 Kwa maana wageni wameinuka dhidi yangu, na watu wasio na huruma wanaitafuta roho yangu; nao hawakumuweka Mungu mbele yao. (Selah)
כי זרים קמו עלי ועריצים בקשו נפשי לא שמו אלהים לנגדם סלה׃
4 Tazama, Mungu ni msaidizi wangu; Bwana ndiye anisaidiaye.
הנה אלהים עזר לי אדני בסמכי נפשי׃
5 Naye atawalipizia uovu maadui zangu; katika uaminifu wako, uwaharibu!
ישוב הרע לשררי באמתך הצמיתם׃
6 Nitakutolea dhabihu kwa moyo mkunjufu; nitalishukuru jina lako, Yahwe, kwa maana ni jema.
בנדבה אזבחה לך אודה שמך יהוה כי טוב׃
7 Kwa kuwa yeye ameniokoa katika kila shida; macho yangu yamewatazama adui zangu yakiwa na ushindi.
כי מכל צרה הצילני ובאיבי ראתה עיני׃

< Zaburi 54 >