< Zaburi 53 >

1 Mpumbavu husema moyoni mwake, “Hakuna Mungu.” Wamepotoka na kufanya machukizo; hakuna mmoja atendaye mema.
“To the chief musician upon Machalath, a Maskil of David.” The worthless fool saith in his heart, There is no God. They are corrupt, and they are abominable [in their] injustice: there is none that doth good.
2 Toka mbinguni Mungu hutazama chini kwa wanadamu kuona kama kuna yeyote mweye akili, amtafutaye yeye.
God looketh down from heaven upon the children of men, to see if there be one intelligent, one who seeketh for God.
3 Wote wamekengeuka. Kwa pamoja wamepotoka. Hakuna atendaye mema, hata mmoja.
Every one [of them] hath departed [from righteousness]; altogether are they become corrupt: there is none that doth good, no, not one.
4 Je, wale wanao fanya uovu hawana uelewa - wale walao watu wangu kana kwamba wanakula mkate na hawamuiti Mungu?
Is there no knowledge in the workers of wickedness? who eat up my people as they eat bread: [while] they do not call on God.
5 Wao walikuwa katika hofu kuu, ingawa hakuna sababu ya kuogopa ilikuwepo hapo; maana Mungu ataitawanya mifupa ya yeyote atakaye kusanyika dhidi yako; watu kama hao wataaibishwa kwa sababu Mungu amewakataa wao.
There were they terrified with terror where there was no terror; for God had scattered the bones of those that encamped against thee: thou didst put them to shame, because God had rejected them.
6 Oh, kwamba wokovu wa Israel ungepatikana Sayuni! Wakati Mungu atakapowaleta watu wake kutoka kifungoni, ndipo Yakobo atashangilia na Israeli itafurahi!
Oh that some one might bring the salvation of Israel out of Zion! When God bringeth back the captivity of his people, [then] will Jacob be glad, [and] Israel will rejoice.

< Zaburi 53 >