< Zaburi 53 >

1 Mpumbavu husema moyoni mwake, “Hakuna Mungu.” Wamepotoka na kufanya machukizo; hakuna mmoja atendaye mema.
Unto the end. For Mahalath: the thoughts of David. The fool has said in his heart, “There is no God.” They were corrupted, and they became abominable with iniquities. There is no one who does good.
2 Toka mbinguni Mungu hutazama chini kwa wanadamu kuona kama kuna yeyote mweye akili, amtafutaye yeye.
God gazed down from heaven on the sons of men, to see if there were any who were considering or seeking God.
3 Wote wamekengeuka. Kwa pamoja wamepotoka. Hakuna atendaye mema, hata mmoja.
All have gone astray; together they have become useless. There is no one who does good; there is not even one.
4 Je, wale wanao fanya uovu hawana uelewa - wale walao watu wangu kana kwamba wanakula mkate na hawamuiti Mungu?
Will they never learn: all those who work iniquity, who devour my people like a meal of bread?
5 Wao walikuwa katika hofu kuu, ingawa hakuna sababu ya kuogopa ilikuwepo hapo; maana Mungu ataitawanya mifupa ya yeyote atakaye kusanyika dhidi yako; watu kama hao wataaibishwa kwa sababu Mungu amewakataa wao.
They have not called upon God. In that place, they have trembled in fear, where there was no fear. For God has scattered the bones of those who please men. They have been confounded, because God has spurned them.
6 Oh, kwamba wokovu wa Israel ungepatikana Sayuni! Wakati Mungu atakapowaleta watu wake kutoka kifungoni, ndipo Yakobo atashangilia na Israeli itafurahi!
Who will grant from Zion the salvation of Israel? Jacob will exult, when God will convert the captivity of his people; and Israel will rejoice.

< Zaburi 53 >