< Zaburi 52 >
1 Kwa nini wewe unajivunia kufanya uovu, wewe mtu mwenye nguvu? Uaminifu wa agano la Mungu huja kila siku.
in finem intellectus David cum venit Doec Idumeus et adnuntiavit Saul et dixit venit David in domo Achimelech quid gloriatur in malitia qui potens est iniquitate
2 Ulimi wako hupanga uharibifu kama wembe mkali, na kufanya udanganyifu.
tota die iniustitiam cogitavit lingua tua sicut novacula acuta fecisti dolum
3 Wewe unapenda uovu kuliko wema na udanganifu kuliko kuongea haki. (Selah)
dilexisti malitiam super benignitatem iniquitatem magis quam loqui aequitatem diapsalma
4 Wewe hupenda maneno ambayo huwaumiza wengine, wewe ulimi mdanganyifu.
dilexisti omnia verba praecipitationis linguam dolosam
5 Vivyo hivyo Mungu atakuadhibu wewe milele; yeye atakuchukua na kukuondoa katika hema yako na kukung'oa katika ardhi ya uhai. (Selah)
propterea Deus destruet te in finem evellet te et emigrabit te de tabernaculo et radicem tuam de terra viventium diapsalma
6 Wenye haki pia wataona na kuogopa; watamcheka na kusema,
videbunt iusti et timebunt et super eum ridebunt et dicent
7 “Tazama, huyu ni mtu ambaye hakumfanya Mungu kuwa kimbilio lake la usalama, bali aliamini katika wingi wa mali zake, naye alikuwa na nguvu alipowaharibu wengine.”
ecce homo qui non posuit Deum adiutorem suum sed speravit in multitudine divitiarum suarum et praevaluit in vanitate sua
8 Lakini kwangu mimi, niko kama mti bora wa mzeituni katika nyumba ya Mungu; Nami nitaamini uaminifu wa agano la Mungu milele na milele.
ego autem sicut oliva fructifera in domo Dei speravi in misericordia Dei in aeternum et in saeculum saeculi
9 Nitakushukuru wewe daima kwa uliyo tenda. Nitalisubiri jina lako, kwa sababu ni zuri, uweponi mwa wantu wako wa kimungu.
confitebor tibi in saeculum quia fecisti et expectabo nomen tuum quoniam bonum in conspectu sanctorum tuorum