< Zaburi 52 >

1 Kwa nini wewe unajivunia kufanya uovu, wewe mtu mwenye nguvu? Uaminifu wa agano la Mungu huja kila siku.
To the chief Musician, Maschil, [A Psalm] of David, when Doeg the Edomite came and told Saul, and said to him, David is come to the house of Ahimelech. Why boastest thou thyself in mischief, O mighty man? the goodness of God [endureth] continually.
2 Ulimi wako hupanga uharibifu kama wembe mkali, na kufanya udanganyifu.
Thy tongue deviseth mischiefs; like a sharp razor, working deceitfully.
3 Wewe unapenda uovu kuliko wema na udanganifu kuliko kuongea haki. (Selah)
Thou lovest evil more than good; [and] lying rather than to speak righteousness. (Selah)
4 Wewe hupenda maneno ambayo huwaumiza wengine, wewe ulimi mdanganyifu.
Thou lovest all devouring words, O [thou] deceitful tongue.
5 Vivyo hivyo Mungu atakuadhibu wewe milele; yeye atakuchukua na kukuondoa katika hema yako na kukung'oa katika ardhi ya uhai. (Selah)
God shall likewise destroy thee for ever, he shall take thee away, and pluck thee out of [thy] dwelling-place, and root thee out of the land of the living. (Selah)
6 Wenye haki pia wataona na kuogopa; watamcheka na kusema,
The righteous also shall see, and fear, and shall laugh at him:
7 “Tazama, huyu ni mtu ambaye hakumfanya Mungu kuwa kimbilio lake la usalama, bali aliamini katika wingi wa mali zake, naye alikuwa na nguvu alipowaharibu wengine.”
Lo, [this is] the man [that] made not God his strength; but trusted in the abundance of his riches, [and] strengthened himself in his wickedness.
8 Lakini kwangu mimi, niko kama mti bora wa mzeituni katika nyumba ya Mungu; Nami nitaamini uaminifu wa agano la Mungu milele na milele.
But I [am] like a green olive tree in the house of God: I trust in the mercy of God for ever and ever.
9 Nitakushukuru wewe daima kwa uliyo tenda. Nitalisubiri jina lako, kwa sababu ni zuri, uweponi mwa wantu wako wa kimungu.
I will praise thee for ever, because thou hast done [it]: and I will wait on thy name; for [it is] good before thy saints.

< Zaburi 52 >