< Zaburi 52 >

1 Kwa nini wewe unajivunia kufanya uovu, wewe mtu mwenye nguvu? Uaminifu wa agano la Mungu huja kila siku.
Why do you boast of mischief, mighty man? God’s chesed ·loving-kindness· endures continually.
2 Ulimi wako hupanga uharibifu kama wembe mkali, na kufanya udanganyifu.
Your tongue plots destruction, like a sharp razor, working deceitfully.
3 Wewe unapenda uovu kuliko wema na udanganifu kuliko kuongea haki. (Selah)
You 'ahavta ·affectionately love· evil more than good, lying rather than speaking the truth. (Selah) ·contemplation with musical interlude·.
4 Wewe hupenda maneno ambayo huwaumiza wengine, wewe ulimi mdanganyifu.
You 'ahavta ·affectionately love· all devouring words, you deceitful tongue.
5 Vivyo hivyo Mungu atakuadhibu wewe milele; yeye atakuchukua na kukuondoa katika hema yako na kukung'oa katika ardhi ya uhai. (Selah)
God will likewise destroy you forever. He will take you up, and pluck you out of your tent, and root you out of the land of the living. (Selah) ·contemplation with musical interlude·.
6 Wenye haki pia wataona na kuogopa; watamcheka na kusema,
The upright also will see it, and fear, and laugh at him, saying,
7 “Tazama, huyu ni mtu ambaye hakumfanya Mungu kuwa kimbilio lake la usalama, bali aliamini katika wingi wa mali zake, naye alikuwa na nguvu alipowaharibu wengine.”
“Behold, this is the man who didn’t make God his strength, but trusted in the abundance of his riches, and strengthened himself in his wickedness.”
8 Lakini kwangu mimi, niko kama mti bora wa mzeituni katika nyumba ya Mungu; Nami nitaamini uaminifu wa agano la Mungu milele na milele.
But as for me, I am like a green olive tree in God’s house. I trust in God’s chesed ·loving-kindness· forever and ever.
9 Nitakushukuru wewe daima kwa uliyo tenda. Nitalisubiri jina lako, kwa sababu ni zuri, uweponi mwa wantu wako wa kimungu.
I will yadah ·extend hands in thankful praise· to you forever, because you have done it. I will hope in your name, for it is good, in the presence of your saints.

< Zaburi 52 >