< Zaburi 51 >

1 Unirehemu, Mungu, kwa sababu ya uaminifu wa agano lako; kwa ajili ya wingi wa matendo yako ya rehema, uyafute makosa yangu.
Al la ĥorestro. Psalmo de David, kiam venis al li la profeto Natan post lia aliĝo al Bat-Ŝeba. Korfavoru min, ho Dio, laŭ Via boneco; Laŭ Via granda kompatemeco elstreku miajn pekojn.
2 Unioshe kabisa uovu wangu na unisafishe dhambi zangu.
Lavu min tute pure de mia krimo, Kaj purigu min de mia peko.
3 Kwa maana ninayajua makosa yangu, na dhambi yangu iko mbele yako siku zote.
Ĉar miajn kulpojn mi konsciadas; Kaj mia peko estas ĉiam antaŭ mi.
4 Dhidi yako, wewe pekee, nimetenda dhambi na kufanya uovu mbele ya macho yako; uko sawa usemapo; wewe uko sahahi utoapo hukumu.
Antaŭ Vi sola mi pekis, Kaj mi faris tion, kio estas malbona antaŭ Viaj okuloj; Tial Vi estas justa en Via vorto Kaj pura en Via juĝo.
5 Tazama, nilizaliwa katika uovu; pindi tu mama yangu aliponibeba mimba, nilikuwa katika dhambi. Tazama, wewe unahitaji uaminifu ndani ya moyo wangu;
Mi estas ja naskita en krimo; Kaj en peko gravediĝis per mi mia patrino.
6 katika moyo wangu wewe utanifanya niijue hekima.
Vi amas ja veron en la koro, Kaj en kaŝiteco Vi aperigas al mi saĝon.
7 Unisafishe kwa hisopo, nami nitakuwa safi; unioshe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
Senpekigu min per hisopo, kaj mi fariĝos pura; Lavu min, kaj mi estos pli blanka ol neĝo.
8 Unifanye kusikia furaha na shangwe ili kwamba mifupa ulioivunja ifurahi.
Aŭdigu al mi ĝojon kaj gajecon, Kaj regajiĝos la ostoj, kiujn Vi batis.
9 Uufiche uso wako mbali na dhambi zangu na uyafute maovu yangu yote.
Kaŝu Vian vizaĝon de miaj pekoj, Kaj ĉiujn miajn krimojn elstreku.
10 Uniumbie moyo safi, Mungu, na uifanye upya roho ya haki ndani yangu.
Koron puran kreu al mi, ho Dio, Kaj spiriton fidelan novigu en mi.
11 Usiniondoe uweponi mwako, na usimuondoe roho Mtakatifu ndani yangu.
Ne forpuŝu min de Via vizaĝo, Kaj Vian sanktan spiriton ne forprenu de mi.
12 Unirudishie furaha ya wokovu wako, na unihifadhi mimi kwa roho ya utayari.
Redonu al mi la ĝojon de Via helpo; Kaj spirito bonfara fortikigu min.
13 Ndipo nitawafundisha wakosaji jia zako, na wenye dhambi watakugeukia wewe.
Mi instruos al la krimuloj Vian vojon; Kaj pekuloj revenos al Vi.
14 Unisamehe kwa ajili ya umwagaji damu, Mungu wa wokovu wangu, nami nitapiga kelele za shangwe ya haki yako.
Liberigu min de sango, ho Dio, Dio de mia savo; Mia lango kantos Vian justecon.
15 Ee Bwana, uifungue midomo yangu, na mdomo wangu itazieleza sifa zako.
Ho, mia Sinjoro, malfermu miajn lipojn; Kaj mia buŝo rakontos Vian gloron.
16 Kwa maana wewe haufurahishwi katika sadaka, vinginevyo ningekutolea sadaka; wewe hauwi radhi katika sadaka ya kuteketezwa.
Ĉar Vi ne deziras oferdonon, alie mi ĝin donus; Brulofero ne plaĉas al Vi.
17 Sadaka ya Mungu ni roho iliyovunjika. Wewe, Mungu hautadharau moyo uliopondeka na kujutia.
Oferdonoj al Dio estas spirito suferanta; Koron suferantan kaj humilan Vi, ho Dio, ne malŝatas.
18 Uitendee mema Sayuni katika nia yako nzuri; uzijenge tena kuta za Yerusalem.
Bonfaru al Cion laŭ Via favoro, Konstruu la murojn de Jerusalem;
19 Kisha wewe utafurahia sadaka yenye haki, katika sadaka za kuteketeza; ndipo watu wetu watatoa ng'ombe kwenye madhabahu yako.
Tiam plaĉos al Vi oferdonoj de pieco, brulofero kaj plenofero; Tiam oni metos sur Vian altaron junajn bovojn.

< Zaburi 51 >