< Zaburi 50 >

1 Mungu, Mwenye nguvu, Yahwe, amenena naye aliita nchi toka mawio ya jua mpaka machweo yake.
Ein Psalm Asafs. / El Elohim Jahwe: Er redet / Und ruft der Erde d vom Aufgang der Sonne bis zum Niedergang.
2 Tokea Sayuni, Mungu ameangaza, ukamilifu wa uzuri.
Aus Zion, der Schönheit Krone, / Strahlt Elohim hervor.
3 Mungu wetu huja naye hakai kimya; mbele yake moto hula, na kuna dhoruba kubwa karibu naye.
Unser Gott, er kommt und schweiget nicht. / Verzehrend Feuer geht vor ihm her, / Rings um ihn stürmt es gewaltig.
4 Yeye huziita mbingu zilizo juu na nchi ili kwamba aweze kuwahukumu watu wake:
Er ruft die Himmel droben herbei. / Und die Erde, sein Volk zu richten:
5 Kwa pamoja kusanyikeni waaminifu wangu kwangu, wale waliofanya nami agano kwa sadaka.”
"Versammelt mir die Frommen, / Die den Bund mit mir im Opfer geschlossen!"
6 Mbingu zitatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ndiye jaji. Serah
Die Himmel künden seine Gerechtigkeit; / Denn Elohim — er ist's, der richtet! (Sela)
7 Sikilizeni, watu wangu, nami nitazungumza; mimi ni Mungu, Mungu wenu.
"Höre, mein Volk, o laß mich reden! / Israel, laß mich dich warnen! / Elohim, dein Gott, bin ich.
8 Sitawakaripia ninyi kwa ajili ya sadaka zenu; sadaka zenu za kuteketeza ziko nami siku zote.
Nicht deiner Schlachtopfer wegen rüge ich dich — / Sind doch deine Brandopfer immer vor mir.
9 Sitachukua ng'ombe katika nyumba yenu, wala beberu katika mazizi yenu.
Nicht brauche ich Stiere aus deinem Hause / Noch Böcke aus deinen Hürden.
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, nao ng'ombe kwenye milima elfu ni wangu.
Denn mein ist alles Wild des Waldes, / Das viele Getier auf den Bergen.
11 Ninawajua ndege wa mlimani, na wanyama pori katika shamba ni wangu.
Ich kenne jeden Vogel der Berge, / Und was auf den Feldern sich regt, ist mein.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi; maana ulimwengu ni wangu, na vyote vilivyomo.
Sollte mich hungern, dir sagte ich's nicht. / Denn mein ist der Erdkreis und was ihn erfüllt.
13 Je! sitakula nyama ya ngombe na kunywa damu ya mbuzi?
Esse ich etwa der Stiere Fleisch / Und trink ich der Böcke Blut?
14 Mtoleeni Mungu sadaka za shukurani, na mlipe viapo vyenu kwa Aliye Juu.
Opfere Elohim Dank / Und bezahle dem Höchsten deine Gelübde!
15 Mniite katika siku ya shida; nami nitawaokoa
"Rufe mich an am Tage der Not: / Dann will ich dich retten, daß du mich ehrest."
16 Lakini kwa waovu Mungu anasema, “Inawahusu nini kuitangaza hali yangu, kwamba ninyi mmeliweka agano langu mdomoni mwenu,
Aber zum Frevler spricht Elohim: / Wie? du zählst meine Satzungen auf / Und redest von meinem Bund?
17 wakati ninyi mnayachukia maelekezo na mnayatupa maneno yangu?
Das wagst du und hasset doch Zucht / Und wirfst meine Worte hinter dich?
18 Mumuanapo mwizi, ninyi hukubaliana naye; ninyi na mnashirikiana na wale wafanyao uasherati.
Siehst du einen Dieb, so gesellst du dich ihm, / Und mit Ehebrechern gehest du um.
19 Mwautoa mdomo wenu kwa mabaya, huelezea udanganyifu.
Du lässest deinen Mund zum Bösen los, / Und deine Zunge spinnet Trug.
20 Mnakaa na kuongea dhidi ya ndugu yenu; na kukashfu mwana wa mama yenu.
Mit andern verleumdest du deinen Bruder, / Deiner Mutter Sohn hängst du Schande an.
21 Mmefanya mambo haya, lakini nimekaa kimya, hivyo mlidhani kuwa ni mtu flani nilliye kama ninyi mlivyo. Lakini nitawakaripia ninyi na kuwafunua, mbele ya macho yenu, mambo yote miliyofanya.
Das hast du getan, und ich schwieg dazu. / Da dachtest du denn: ich wäre wie du. / Aber ich will dich zur Rechenschaft ziehn, / Dir's unter die Augen stellen."
22 Mlitilie maanani hili, ninyi mnao msahau Mungu, vinginevyo nitawakata ninyi vipande vipande, na hatakuwepo yeyote wakuja kuwasaidia!
Merkt das wohl, die ihr Gottes vergeßt; / Sonst werd ich zerreißen, und niemand rettet.
23 Yule atoaye sadaka ya shukurani hunitukuza, na yeyote apangaye njia zake katika namna iliyo sahihi nitamuonesha wokovu wa Mungu.”
Wer Dank opfert, der ehret mich recht, / Und er bahnet den Weg, / Auf dem ich ihm zeige das Heil Elohims.

< Zaburi 50 >