< Zaburi 50 >

1 Mungu, Mwenye nguvu, Yahwe, amenena naye aliita nchi toka mawio ya jua mpaka machweo yake.
Psaume d'Asaph. Le Dieu des dieux, le Seigneur a parlé, et il a appelé la terre depuis l'Orient jusqu'à l'Occident
2 Tokea Sayuni, Mungu ameangaza, ukamilifu wa uzuri.
De Sion vient la splendeur de sa beauté.
3 Mungu wetu huja naye hakai kimya; mbele yake moto hula, na kuna dhoruba kubwa karibu naye.
Dieu, notre Dieu viendra manifestement, et ne gardera pas le silence; un feu sera allume en sa présence, et tout alentour un vent impétueux soufflera.
4 Yeye huziita mbingu zilizo juu na nchi ili kwamba aweze kuwahukumu watu wake:
Il convoquera le ciel et la terre, pour juger son peuple.
5 Kwa pamoja kusanyikeni waaminifu wangu kwangu, wale waliofanya nami agano kwa sadaka.”
Amenez-lui ses saints, ceux qui ont fait alliance avec lui, pour les sacrifices.
6 Mbingu zitatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ndiye jaji. Serah
Et les cieux annonceront sa justice; car Dieu est le juge.
7 Sikilizeni, watu wangu, nami nitazungumza; mimi ni Mungu, Mungu wenu.
Écoute, mon peuple, et je parlerai; Israël, je te l'atteste: je suis Dieu, je suis ton Dieu.
8 Sitawakaripia ninyi kwa ajili ya sadaka zenu; sadaka zenu za kuteketeza ziko nami siku zote.
Je ne te réprimanderai point sur tes sacrifices; car tes holocaustes sont toujours devant mes yeux.
9 Sitachukua ng'ombe katika nyumba yenu, wala beberu katika mazizi yenu.
Je ne prendrai pas de bœufs de ta maison, ni de boucs de tes menus troupeaux.
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, nao ng'ombe kwenye milima elfu ni wangu.
Car toutes les bêtes de la forêt m'appartiennent, et le bétail des montagnes et les taureaux.
11 Ninawajua ndege wa mlimani, na wanyama pori katika shamba ni wangu.
Je connais tous les oiseaux du ciel, et la beauté des champs est à moi.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi; maana ulimwengu ni wangu, na vyote vilivyomo.
Si j'ai faim, je ne te le dis pas; car toute la terre habitée m'appartient et sa plénitude.
13 Je! sitakula nyama ya ngombe na kunywa damu ya mbuzi?
Est-ce que je mange la chair des taureaux? est-ce que je bois le sang des boucs?
14 Mtoleeni Mungu sadaka za shukurani, na mlipe viapo vyenu kwa Aliye Juu.
Immole à Dieu une victime de louanges; rends au Tout-Puissant tes vœux.
15 Mniite katika siku ya shida; nami nitawaokoa
Invoque-moi au jour de l'affliction, et je te sauverai, et tu me rendras grâces.
16 Lakini kwa waovu Mungu anasema, “Inawahusu nini kuitangaza hali yangu, kwamba ninyi mmeliweka agano langu mdomoni mwenu,
Mais Dieu a dit au pécheur: Pourquoi publies-tu mes justices et as-tu mon alliance à la bouche,
17 wakati ninyi mnayachukia maelekezo na mnayatupa maneno yangu?
Quand tu n'aimes point ma discipline, et que tu as rejeté loin de toi ma parole?
18 Mumuanapo mwizi, ninyi hukubaliana naye; ninyi na mnashirikiana na wale wafanyao uasherati.
Si tu voyais un larron, tu courais avec lui; tu avais ta part avec les adultères;
19 Mwautoa mdomo wenu kwa mabaya, huelezea udanganyifu.
Ta bouche abondait en méchanceté, et ta langue tramait la fraude.
20 Mnakaa na kuongea dhidi ya ndugu yenu; na kukashfu mwana wa mama yenu.
Assis, tu médisais de ton frère; tu scandalisais le fils de ta mère.
21 Mmefanya mambo haya, lakini nimekaa kimya, hivyo mlidhani kuwa ni mtu flani nilliye kama ninyi mlivyo. Lakini nitawakaripia ninyi na kuwafunua, mbele ya macho yenu, mambo yote miliyofanya.
Voilà ce que tu faisais, et j'ai gardé le silence; mais tu t'imaginais faussement que je serais semblable à toi. Je te convaincrai, et je mettrai tes offenses devant ta face.
22 Mlitilie maanani hili, ninyi mnao msahau Mungu, vinginevyo nitawakata ninyi vipande vipande, na hatakuwepo yeyote wakuja kuwasaidia!
Comprenez donc ces choses, vous qui oubliez Dieu; de peur qu'un jour il ne vous ravisse, et que nul ne vous délivre.
23 Yule atoaye sadaka ya shukurani hunitukuza, na yeyote apangaye njia zake katika namna iliyo sahihi nitamuonesha wokovu wa Mungu.”
C'est un sacrifice de louange qui m'honore, et la voie où je montrerai le salut de Dieu.

< Zaburi 50 >