< Zaburi 5 >
1 Sikiliza nikuitapo, Yahweh; tazama kuugua kwangu.
“For the leader of the music; to be accompanied with wind instruments. A psalm of David.” Give ear to my words, O LORD; Have regard to my cry!
2 Sikiliza sauti yangu nikuitapo, Ee Mfalme wangu na Mungu wangu, kwa kuwa ni kwako Bwana naomba.
Listen to the voice of my supplication, my King and my God! For to thee do I address my prayer.
3 Yahweh; sikia kilio changu asubuhi; na asubuhi nitaleta dua yangu kwako na kungoja kwa matarajio.
In the morning shalt thou hear my voice, O LORD! In the morning will I address my prayer to thee, and look for help.
4 Hakika wewe ni Mungu usiye kubaliana na uovu; watu waovu hawawezi kuwa wageni wako.
For thou art not a God that hath pleasure in wickedness; The unrighteous man dwelleth not with thee.
5 Wenye kiburi hawata simama katika uwepo wako; wewe unawachukia wote wanaofanya maovu.
The haughty shall not stand in thy sight; Thou hatest all that do iniquity.
6 Nawe utawaharibu waongo; Yahweh huwadharau vurugu na watu wadanganyifu.
Thou destroyest them that speak falsehood; The man of blood and deceit the LORD abhorreth.
7 Lakini kwangu mimi, kwa sababu ya ukuu na uaminifu wa agano lako, nitakuja nyumbani mwako; na kwa heshima nitakuinamia mbele ya hekalu lako takatifu.
But I, through thy great goodness, will come to thy house; In thy fear will I worship at thy holy temple.
8 Oh Bwana, uniongoze katika haki yako kwa sababu ya adui zangu; usawazishe njia yako mbele yangu.
Lead me, O LORD! in thy righteousness, because of mine enemies; Make thy path straight before my face!
9 Kwa kuwa midomoni mwao hamna ukweli; utu wao wa ndani ni mwovu; makoo yao ni kaburi lililo wazi; husifu kinafiki kwa ulimi wao.
For in their mouth there is no truth; Their heart is malignity; Their throat is an open sepulchre; They flatter with their tongue.
10 Mungu, wafanye kuwa na hatia; mipango yao iwe kuanguka kwao! Kwa ajili ya makosa yao mengi uwatoe nje, kwa kuwa wamekuasi wewe.
Requite them, O God! Let them be confounded in their devices; Cast them out for the multitude of their transgressions; For against thee have they rebelled!
11 Bali wale wanao kukimbilia wafurahi; uwafanye wapige kelele kwa shangwe siku zote kwa sababu unawapigania; uwafanye wenye furaha ndani yako, wale walipendao jina lako.
But let all, that put their trust in thee, rejoice; Let them ever shout for joy, because thou defendest them; Let them, that love thy name, be joyful in thee!
12 Kwa maana utawabariki wenye haki, Yahweh; utawazunguka kwa neema kama ngao.
For thou, O LORD! dost bless the righteous; With favor dost thou encompass him, as with a shield.