< Zaburi 5 >
1 Sikiliza nikuitapo, Yahweh; tazama kuugua kwangu.
[For the Chief Musician, with the flutes. A Psalm by David.] Listen to my words, LORD. Consider my (meditation)
2 Sikiliza sauti yangu nikuitapo, Ee Mfalme wangu na Mungu wangu, kwa kuwa ni kwako Bwana naomba.
Give attention to the voice of my cry, my King and my God; for to you do I pray.
3 Yahweh; sikia kilio changu asubuhi; na asubuhi nitaleta dua yangu kwako na kungoja kwa matarajio.
LORD, in the morning you shall hear my voice. In the morning I will lay my requests before you, and watch.
4 Hakika wewe ni Mungu usiye kubaliana na uovu; watu waovu hawawezi kuwa wageni wako.
For you are not a God who desires wickedness. Evil can't live with you.
5 Wenye kiburi hawata simama katika uwepo wako; wewe unawachukia wote wanaofanya maovu.
The arrogant shall not stand in your sight. You hate all evildoers.
6 Nawe utawaharibu waongo; Yahweh huwadharau vurugu na watu wadanganyifu.
You will destroy those who speak lies. The LORD despises a person of bloodshed and deceit.
7 Lakini kwangu mimi, kwa sababu ya ukuu na uaminifu wa agano lako, nitakuja nyumbani mwako; na kwa heshima nitakuinamia mbele ya hekalu lako takatifu.
But as for me, in the abundance of your loving kindness I will enter into your house. I will bow toward your holy temple in reverence of you.
8 Oh Bwana, uniongoze katika haki yako kwa sababu ya adui zangu; usawazishe njia yako mbele yangu.
Lead me, LORD, in your righteousness because of my enemies. Make your way straight before me.
9 Kwa kuwa midomoni mwao hamna ukweli; utu wao wa ndani ni mwovu; makoo yao ni kaburi lililo wazi; husifu kinafiki kwa ulimi wao.
For there is nothing reliable in their mouth. Their heart is destruction. Their throat is an open tomb; with their tongues they flatter.
10 Mungu, wafanye kuwa na hatia; mipango yao iwe kuanguka kwao! Kwa ajili ya makosa yao mengi uwatoe nje, kwa kuwa wamekuasi wewe.
Hold them guilty, God. Let them fall by their own counsels. Cast them out because of the multitude of their transgressions, for they have rebelled against you.
11 Bali wale wanao kukimbilia wafurahi; uwafanye wapige kelele kwa shangwe siku zote kwa sababu unawapigania; uwafanye wenye furaha ndani yako, wale walipendao jina lako.
But let all those who take refuge in you rejoice. Let them always shout for joy, because you defend them. And let those who love your name be joyful in you.
12 Kwa maana utawabariki wenye haki, Yahweh; utawazunguka kwa neema kama ngao.
For you bless the righteous, LORD. You surround him with favor like a shield.