< Zaburi 5 >

1 Sikiliza nikuitapo, Yahweh; tazama kuugua kwangu.
For the Leader; upon the Nehiloth. A Psalm of David. Give ear to my words, O LORD, consider my (meditation)
2 Sikiliza sauti yangu nikuitapo, Ee Mfalme wangu na Mungu wangu, kwa kuwa ni kwako Bwana naomba.
Hearken unto the voice of my cry, my King, and my God; for unto Thee do I pray.
3 Yahweh; sikia kilio changu asubuhi; na asubuhi nitaleta dua yangu kwako na kungoja kwa matarajio.
O LORD, in the morning shalt Thou hear my voice; in the morning will I order my prayer unto Thee, and will look forward.
4 Hakika wewe ni Mungu usiye kubaliana na uovu; watu waovu hawawezi kuwa wageni wako.
For Thou art not a God that hath pleasure in wickedness; evil shall not sojourn with Thee.
5 Wenye kiburi hawata simama katika uwepo wako; wewe unawachukia wote wanaofanya maovu.
The boasters shall not stand in Thy sight; Thou hatest all workers of iniquity.
6 Nawe utawaharibu waongo; Yahweh huwadharau vurugu na watu wadanganyifu.
Thou destroyest them that speak falsehood; the LORD abhorreth the man of blood and of deceit.
7 Lakini kwangu mimi, kwa sababu ya ukuu na uaminifu wa agano lako, nitakuja nyumbani mwako; na kwa heshima nitakuinamia mbele ya hekalu lako takatifu.
But as for me, in the abundance of Thy lovingkindness will I come into Thy house; I will bow down toward Thy holy temple in the fear of Thee.
8 Oh Bwana, uniongoze katika haki yako kwa sababu ya adui zangu; usawazishe njia yako mbele yangu.
O LORD, lead me in Thy righteousness because of them that lie in wait for me; make Thy way straight before my face.
9 Kwa kuwa midomoni mwao hamna ukweli; utu wao wa ndani ni mwovu; makoo yao ni kaburi lililo wazi; husifu kinafiki kwa ulimi wao.
For there is no sincerity in their mouth; their inward part is a yawning gulf, their throat is an open sepulchre; they make smooth their tongue.
10 Mungu, wafanye kuwa na hatia; mipango yao iwe kuanguka kwao! Kwa ajili ya makosa yao mengi uwatoe nje, kwa kuwa wamekuasi wewe.
Hold them guilty, O God, let them fall by their own counsels; cast them down in the multitude of their transgressions; for they have rebelled against Thee.
11 Bali wale wanao kukimbilia wafurahi; uwafanye wapige kelele kwa shangwe siku zote kwa sababu unawapigania; uwafanye wenye furaha ndani yako, wale walipendao jina lako.
So shall all those that take refuge in Thee rejoice, they shall ever shout for joy, and Thou shalt shelter them; let them also that love Thy name exult in Thee.
12 Kwa maana utawabariki wenye haki, Yahweh; utawazunguka kwa neema kama ngao.
For Thou dost bless the righteous; O LORD, Thou dost encompass him with favour as with a shield.

< Zaburi 5 >