< Zaburi 49 >
1 Sikieni hili, ninyi watu wote; tegeni masikio, ninyi wenyeji wa dunia,
“For the leader of the music. A psalm of the sons of Korah.” Hear this, all ye nations; Give ear, all ye inhabitants of the world;
2 wote walio chini na walio juu, tajiri na masikini wote pamoja.
Both high and low, rich and poor alike!
3 Mdomo wangu utazungumza hekima na tafakari ya moyo wangu itakuwa ya uelewa.
My mouth shall speak wisdom, And the meditation of my mind shall be understanding.
4 Nitaelekeza sikio langu kwenye mfano; nitaanza mfano wangu kwa kinubi.
I will incline mine ear to a poem; I will utter my song upon the harp.
5 Kwa nini nilazimike kuziogopa siku za uovu, wakati uovu umenizunguka kwenye visigino vyangu?
Why should I fear in the days of adversity, When the iniquity of my adversaries encompasseth me;
6 Kwa nini niwaogope wale wanao amini katika mali zao na kujivuna kuhusu utajiri wao?
They who trust in their riches, And glory in the greatness of their wealth?
7 Ni hakika kuwa hakuna yeyote atakaye muokoa ndugu yake au kumpa Mungu pesa kwa ajili yake,
No one can redeem his brother from death, Nor give a ransom for him to God,
8 Kwa maana ukombozi wa uhai wa mtu ni gharama kubwa, na hakuna awezaye kulipa kile tunacho daiwa.
That he should live to eternity, And not see the pit.
9 Hakuna yeyote atakaye ishi milele ili mwili wake usioze.
Too costly is the redemption of his life, And he giveth it up for ever.
10 Maana yeye ataona uozo. Watu wenye hekima hufa; wajinga pia huangamia na kuacha mali zao kwa wengine.
For he seeth that wise men die, As well as the foolish and the ignorant; They perish alike, And leave their wealth to others.
11 Mawazo yao ya ndani ni kuwa familia zao zitaishi milele, na mahali waishipo, kwa vizazi vyote; wanaita ardhi zao kwa majina yao wenyewe.
They imagine that their houses will endure for ever, And their dwelling-places from generation to generation: Men celebrate their names on the earth.
12 Lakini mtu, kuwa na mali, haimaanishi atabaki hai; kama wanyama walioangamia.
Yet man, who is in honor, abideth not; He is like the beasts that perish.
13 Hii ni hatma ya wafanyao ujinga baada ya kufa, .................
Such is the way which is their confidence! And they who come after them approve their maxims. (Pause)
14 Kama kondoo wamechaguliwa kwa ajili ya kuzimu na kifo kitakuwa mchungaji wao. Nao watatawaliwa na wenye haki ifikapo asubuhi, na miili yao italiwa kuzimuni, wakiwa hawana afasi ya kuishi kwa ajili yao. (Sheol )
Like sheep they are cast into the underworld; Death shall feed upon them; And the upright shall soon trample upon them. Their form shall be consumed in the underworld, And they shall no more have a dwelling-place. (Sheol )
15 Bali Mungu ataufufua uhai wangu kutoka katika nguvu ya kuzimu; naye atanipokea. (Selah) (Sheol )
But God will redeem my life from the underworld; Yea, he will take me under his care. (Pause) (Sheol )
16 Msifadhaike mtu awapo tajiri, utukufu wa nyumba yake uongezekapo.
Be not thou afraid, when one becometh rich; When the glory of his house is increased!
17 Maana atakapo kufa hataondoka na chochote; utukufu wake hautamfuata yeye.
For, when he dieth, he will carry nothing away; His glory will not descend after him.
18 Yeye huifurahisha nafsi yake awapo hai na watu hukusifu wewe uishipo maisha yako mwenyewe-
Though in his life he thought himself happy, —Though men praised thee, while thou wast in prosperity, —
19 naye atakwenda kwenye ukoo wa baba zake naye kamwe hataiona nuru tena.
Yet shalt thou go to the dwelling-place of thy fathers, Who never more shall see the light!
20 Yule ambaye ana mali lakini hana ufahamu ni kama wanyama, ambao wataangamia.
The man who is in honor, but without understanding, Is like the beasts that perish.