< Zaburi 49 >
1 Sikieni hili, ninyi watu wote; tegeni masikio, ninyi wenyeji wa dunia,
TO THE OVERSEER. A PSALM OF THE SONS OF KORAH. Hear this, all you peoples, Give ear, all you inhabitants of the world.
2 wote walio chini na walio juu, tajiri na masikini wote pamoja.
Both low and high, together rich and needy.
3 Mdomo wangu utazungumza hekima na tafakari ya moyo wangu itakuwa ya uelewa.
My mouth speaks wise things, And the meditations of my heart [are] things of understanding.
4 Nitaelekeza sikio langu kwenye mfano; nitaanza mfano wangu kwa kinubi.
I incline my ear to an allegory, I open my riddle with a harp:
5 Kwa nini nilazimike kuziogopa siku za uovu, wakati uovu umenizunguka kwenye visigino vyangu?
Why do I fear in days of evil? The iniquity of my supplanters surrounds me.
6 Kwa nini niwaogope wale wanao amini katika mali zao na kujivuna kuhusu utajiri wao?
Those trusting on their wealth, And in the multitude of their riches, Show themselves foolish.
7 Ni hakika kuwa hakuna yeyote atakaye muokoa ndugu yake au kumpa Mungu pesa kwa ajili yake,
A brother ransoms no one at all, He does not give to God his atonement.
8 Kwa maana ukombozi wa uhai wa mtu ni gharama kubwa, na hakuna awezaye kulipa kile tunacho daiwa.
And precious [is] the redemption of their soul, And it has ceased for all time.
9 Hakuna yeyote atakaye ishi milele ili mwili wake usioze.
And still he lives forever, He does not see the pit.
10 Maana yeye ataona uozo. Watu wenye hekima hufa; wajinga pia huangamia na kuacha mali zao kwa wengine.
For he sees wise men die, Together the foolish and brutish perish, And have left their wealth to others.
11 Mawazo yao ya ndani ni kuwa familia zao zitaishi milele, na mahali waishipo, kwa vizazi vyote; wanaita ardhi zao kwa majina yao wenyewe.
Their heart [is that] their houses [are] for all time, Their dwelling places from generation to generation. They proclaimed their names over the lands.
12 Lakini mtu, kuwa na mali, haimaanishi atabaki hai; kama wanyama walioangamia.
And man does not remain in honor, He has been like the beasts, they have been cut off.
13 Hii ni hatma ya wafanyao ujinga baada ya kufa, .................
This their way [is] folly for them, And their posterity are pleased with their sayings. (Selah)
14 Kama kondoo wamechaguliwa kwa ajili ya kuzimu na kifo kitakuwa mchungaji wao. Nao watatawaliwa na wenye haki ifikapo asubuhi, na miili yao italiwa kuzimuni, wakiwa hawana afasi ya kuishi kwa ajili yao. (Sheol )
They have set themselves as sheep for Sheol, Death afflicts them, And the upright rule over them in the morning, And their form [is] for consumption. Sheol [is] a dwelling for him. (Sheol )
15 Bali Mungu ataufufua uhai wangu kutoka katika nguvu ya kuzimu; naye atanipokea. (Selah) (Sheol )
Only, God ransoms my soul from the hand of Sheol, For He receives me. (Selah) (Sheol )
16 Msifadhaike mtu awapo tajiri, utukufu wa nyumba yake uongezekapo.
Do not fear when one makes wealth, When the glory of his house is abundant,
17 Maana atakapo kufa hataondoka na chochote; utukufu wake hautamfuata yeye.
For at his death he receives nothing, His glory does not go down after him.
18 Yeye huifurahisha nafsi yake awapo hai na watu hukusifu wewe uishipo maisha yako mwenyewe-
For he blesses his soul in his life (And they praise you when you do well for yourself).
19 naye atakwenda kwenye ukoo wa baba zake naye kamwe hataiona nuru tena.
It comes to the generation of his fathers, They do not see the light forever.
20 Yule ambaye ana mali lakini hana ufahamu ni kama wanyama, ambao wataangamia.
Man in honor, who does not understand, Has been like the beasts, they have been cut off!