< Zaburi 49 >

1 Sikieni hili, ninyi watu wote; tegeni masikio, ninyi wenyeji wa dunia,
For the end, a Psalm for the sons of Core. Hear these words, all you nations, listen, all you that dwell upon the earth:
2 wote walio chini na walio juu, tajiri na masikini wote pamoja.
both the sons of mean men, and sons of [great] men; the rich and poor [man] together.
3 Mdomo wangu utazungumza hekima na tafakari ya moyo wangu itakuwa ya uelewa.
My mouth shall speak of wisdom; and the meditation of my heart shall bring [forth] understanding.
4 Nitaelekeza sikio langu kwenye mfano; nitaanza mfano wangu kwa kinubi.
I will incline mine ear to a parable: I will open my riddle on the harp.
5 Kwa nini nilazimike kuziogopa siku za uovu, wakati uovu umenizunguka kwenye visigino vyangu?
Therefore should I fear in the evil day? the iniquity of my heel shall compass me.
6 Kwa nini niwaogope wale wanao amini katika mali zao na kujivuna kuhusu utajiri wao?
They that trust in their strength, and boast themselves in the multitude of their wealth—
7 Ni hakika kuwa hakuna yeyote atakaye muokoa ndugu yake au kumpa Mungu pesa kwa ajili yake,
A brother does not redeem, shall a man redeem? he shall not give to God a ransom for himself,
8 Kwa maana ukombozi wa uhai wa mtu ni gharama kubwa, na hakuna awezaye kulipa kile tunacho daiwa.
or the price of the redemption of his soul, though he labor for ever,
9 Hakuna yeyote atakaye ishi milele ili mwili wake usioze.
and live to the end, [so] that he should not see corruption.
10 Maana yeye ataona uozo. Watu wenye hekima hufa; wajinga pia huangamia na kuacha mali zao kwa wengine.
When he shall see wise men dying, the fool and the senseless one shall perish together; and they shall leave their wealth to strangers.
11 Mawazo yao ya ndani ni kuwa familia zao zitaishi milele, na mahali waishipo, kwa vizazi vyote; wanaita ardhi zao kwa majina yao wenyewe.
And their sepulchres are their houses for ever, [even] their tabernacles to all generations: they have called their lands after their own names.
12 Lakini mtu, kuwa na mali, haimaanishi atabaki hai; kama wanyama walioangamia.
And man being in honor, understands not: he is compared to the senseless cattle, and is like to them.
13 Hii ni hatma ya wafanyao ujinga baada ya kufa, .................
This their way is an offense to them: yet afterwards men will commend their sayings. (Pause)
14 Kama kondoo wamechaguliwa kwa ajili ya kuzimu na kifo kitakuwa mchungaji wao. Nao watatawaliwa na wenye haki ifikapo asubuhi, na miili yao italiwa kuzimuni, wakiwa hawana afasi ya kuishi kwa ajili yao. (Sheol h7585)
They have laid [them] as sheep in Hades; death shall feed on them; and the upright shall have dominion over them in the morning, and their help shall fail in Hades from their glory. (Sheol h7585)
15 Bali Mungu ataufufua uhai wangu kutoka katika nguvu ya kuzimu; naye atanipokea. (Selah) (Sheol h7585)
But God shall deliver my soul from the power of Hades, when he shall receive me. (Pause) (Sheol h7585)
16 Msifadhaike mtu awapo tajiri, utukufu wa nyumba yake uongezekapo.
Fear not when a man is enriched, and when the glory of his house is increased.
17 Maana atakapo kufa hataondoka na chochote; utukufu wake hautamfuata yeye.
For he shall take nothing when he dies; neither shall his glory descend with him.
18 Yeye huifurahisha nafsi yake awapo hai na watu hukusifu wewe uishipo maisha yako mwenyewe-
For his soul shall be blessed in his life: he shall give thanks to you when you do well to him.
19 naye atakwenda kwenye ukoo wa baba zake naye kamwe hataiona nuru tena.
[Yet] he shall go in to the generation of his fathers; he shall never see light.
20 Yule ambaye ana mali lakini hana ufahamu ni kama wanyama, ambao wataangamia.
Man that is in honor, understands not: he is compared to the senseless cattle, and is like them.

< Zaburi 49 >