< Zaburi 49 >
1 Sikieni hili, ninyi watu wote; tegeni masikio, ninyi wenyeji wa dunia,
For the Leader; a Psalm of the sons of Korah. Hear this, all ye peoples; give ear, all ye inhabitants of the world,
2 wote walio chini na walio juu, tajiri na masikini wote pamoja.
Both low and high, rich and poor together.
3 Mdomo wangu utazungumza hekima na tafakari ya moyo wangu itakuwa ya uelewa.
My mouth shall speak wisdom, and the meditation of my heart shall be understanding.
4 Nitaelekeza sikio langu kwenye mfano; nitaanza mfano wangu kwa kinubi.
I will incline mine ear to a parable; I will open my dark saying upon the harp.
5 Kwa nini nilazimike kuziogopa siku za uovu, wakati uovu umenizunguka kwenye visigino vyangu?
Wherefore should I fear in the days of evil, when the iniquity of my supplanters compasseth me about,
6 Kwa nini niwaogope wale wanao amini katika mali zao na kujivuna kuhusu utajiri wao?
Of them that trust in their wealth, and boast themselves in the multitude of their riches?
7 Ni hakika kuwa hakuna yeyote atakaye muokoa ndugu yake au kumpa Mungu pesa kwa ajili yake,
No man can by any means redeem his brother, nor give to God a ransom for him —
8 Kwa maana ukombozi wa uhai wa mtu ni gharama kubwa, na hakuna awezaye kulipa kile tunacho daiwa.
For too costly is the redemption of their soul, and must be let alone for ever —
9 Hakuna yeyote atakaye ishi milele ili mwili wake usioze.
That he should still live alway, that he should not see the pit.
10 Maana yeye ataona uozo. Watu wenye hekima hufa; wajinga pia huangamia na kuacha mali zao kwa wengine.
For he seeth that wise men die, the fool and the brutish together perish, and leave their wealth to others.
11 Mawazo yao ya ndani ni kuwa familia zao zitaishi milele, na mahali waishipo, kwa vizazi vyote; wanaita ardhi zao kwa majina yao wenyewe.
Their inward thought is, that their houses shall continue for ever, and their dwelling-places to all generations; they call their lands after their own names.
12 Lakini mtu, kuwa na mali, haimaanishi atabaki hai; kama wanyama walioangamia.
But man abideth not in honour; he is like the beasts that perish.
13 Hii ni hatma ya wafanyao ujinga baada ya kufa, .................
This is the way of them that are foolish, and of those who after them approve their sayings. (Selah)
14 Kama kondoo wamechaguliwa kwa ajili ya kuzimu na kifo kitakuwa mchungaji wao. Nao watatawaliwa na wenye haki ifikapo asubuhi, na miili yao italiwa kuzimuni, wakiwa hawana afasi ya kuishi kwa ajili yao. (Sheol )
Like sheep they are appointed for the nether-world; death shall be their shepherd; and the upright shall have dominion over them in the morning; and their form shall be for the nether-world to wear away, that there be no habitation for it. (Sheol )
15 Bali Mungu ataufufua uhai wangu kutoka katika nguvu ya kuzimu; naye atanipokea. (Selah) (Sheol )
But God will redeem my soul from the power of the nether-world; for He shall receive me. (Selah) (Sheol )
16 Msifadhaike mtu awapo tajiri, utukufu wa nyumba yake uongezekapo.
Be not thou afraid when one waxeth rich, when the wealth of his house is increased;
17 Maana atakapo kufa hataondoka na chochote; utukufu wake hautamfuata yeye.
For when he dieth he shall carry nothing away; his wealth shall not descend after him.
18 Yeye huifurahisha nafsi yake awapo hai na watu hukusifu wewe uishipo maisha yako mwenyewe-
Though while he lived he blessed his soul: 'Men will praise thee, when thou shalt do well to thyself';
19 naye atakwenda kwenye ukoo wa baba zake naye kamwe hataiona nuru tena.
It shall go to the generation of his fathers; they shall never see the light.
20 Yule ambaye ana mali lakini hana ufahamu ni kama wanyama, ambao wataangamia.
Man that is in honour understandeth not; he is like the beasts that perish.