< Zaburi 48 >

1 Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
Grande es Jehová, y digno de ser en grande manera alabado en la ciudad de nuestro Dios, en el monte de su santuario.
2 Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
De hermosa situación, el gozo de toda la tierra es el monte de Sión: los lados del aquilón, la ciudad del gran Rey.
3 Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
Dios en sus palacios es conocido por refugio.
4 Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
Porque, he aquí, los reyes de la tierra fueron congregados; pasaron todos.
5 Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
Ellos vieron, maravilláronse grandemente, fueron asombrados: diéronse priesa.
6 Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
Temblor los tomó allí; dolor, como a mujer que pare.
7 Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
Con viento solano quiebras las naves de Társis.
8 Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
Como lo oímos, así lo vimos en la ciudad de Jehová de los ejércitos, en la ciudad de nuestro Dios: Dios la afirmará para siempre. (Selah)
9 Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
Esperamos, o! Dios, tu misericordia en medio de tu templo.
10 Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
Conforme a tu nombre, o! Dios, así es tu loor hasta los fines de la tierra: de justicia está llena tu diestra.
11 Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
Alegrarse ha el monte de Sión: regocijarse han las hijas de Judá por tus juicios.
12 Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
Rodeád a Sión, y cercádla: contád sus torres.
13 mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
Ponéd vuestro corazón a su antemuro: mirád sus palacios, para que lo contéis a la generación que vendrá.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.
Porque este Dios es Dios nuestro eternalmente y para siempre: él nos capitaneará hasta la muerte.

< Zaburi 48 >