< Zaburi 48 >

1 Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
Una canción. Un salmo de los hijos de Coré. Grande es Yahvé, y digno de gran alabanza, en la ciudad de nuestro Dios, en su santo monte.
2 Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
Hermoso en elevación, la alegría de toda la tierra, es el Monte Zion, en los lados norte, la ciudad del gran Rey.
3 Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
Dios se ha mostrado en sus ciudadelas como un refugio.
4 Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
Pues he aquí que los reyes se han reunido, pasaron juntos.
5 Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
Lo vieron y se asombraron. Estaban consternados. Se apresuraron a marcharse.
6 Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
El temblor se apoderó de ellos allí, dolor, como el de una mujer de parto.
7 Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
Con el viento del este, rompes las naves de Tarsis.
8 Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
Como hemos oído, hemos visto, en la ciudad de Yahvé de los Ejércitos, en la ciudad de nuestro Dios. Dios lo establecerá para siempre. (Selah)
9 Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
Hemos pensado en tu amorosa bondad, Dios, en el centro de su templo.
10 Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
Como tu nombre, Dios, así es tu alabanza hasta los confines de la tierra. Tu mano derecha está llena de justicia.
11 Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
¡Que se alegre el monte Sión! Que las hijas de Judá se alegren por tus juicios.
12 Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
Camina alrededor de Sión y rodéala. Numerar sus torres.
13 mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
Fíjate en sus baluartes. Considera sus palacios, para que lo cuentes a la siguiente generación.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.
Porque este Dios es nuestro Dios por los siglos de los siglos. Él será nuestro guía incluso hasta la muerte.

< Zaburi 48 >