< Zaburi 48 >

1 Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
Grande é o Senhor e mui digno de louvor, na cidade do nosso Deus, no seu monte santo.
2 Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
Formoso de sítio, e alegria de toda a terra é o monte de Sião sobre os lados do norte, a cidade do grande Rei.
3 Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
Deus é conhecido nos seus palácios por um alto refúgio.
4 Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
Porque eis que os reis se ajuntaram: eles passaram juntos.
5 Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
Viram-no, e ficaram maravilhados; ficaram assombrados e se apressaram em fugir.
6 Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
Tremor ali os tomou, e dores como de mulher de parto.
7 Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
Tu quebras as naus de Tarsis com um vento oriental.
8 Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
Como o ouvimos, assim o vimos na cidade do Senhor dos exércitos, na cidade do nosso Deus. Deus a confirmará para sempre (Selah)
9 Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
Lembramo-nos, ó Deus, da tua benignidade no meio do teu templo.
10 Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
Segundo é o teu nome, ó Deus, assim é o teu louvor, até aos fins da terra: a tua mão direita está cheia de justiça.
11 Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
Alegre-se o monte de Sião; alegrem-se as filhas de Judá por causa dos teus juízos.
12 Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
Rodeai Sião, e cercai-a, contai as suas torres.
13 mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
Marcai bem os seus antemuros, considerai os seus palácios, para que o conteis à geração seguinte.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.
Porque este Deus é o nosso Deus para sempre, ele será nosso guia até à morte.

< Zaburi 48 >