< Zaburi 48 >
1 Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
Cantique. Psaume des fils de Coré. Yahweh est grand, il est l’objet de toute louange, dans la cité de notre Dieu, sur sa montagne sainte.
2 Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
Elle s’élève gracieuse, joie de toute la terre, la montagne de Sion, aux extrémités du septentrion, la cité du grand Roi.
3 Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
Dieu, dans ses palais, s’est fait connaître comme un refuge.
4 Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
Car voici que les rois s’étaient réunis, ensemble ils s’étaient avancés.
5 Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
Ils ont vu, soudain ils ont été dans la stupeur; éperdus, ils ont pris la fuite.
6 Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
Là un tremblement les a saisis, une douleur comme celle de la femme qui enfante.
7 Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
Par le vent d’Orient tu brises les vaisseaux de Tharsis.
8 Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
Ce que nous avions entendu dire, nous l’avons vu dans la cité de Yahweh des armées; dans la cité de notre Dieu: Dieu l’affermit pour toujours. — Séla.
9 Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
O Dieu nous rappelons la mémoire de ta bonté, au milieu de ton temple.
10 Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
Comme ton nom, ô Dieu, ainsi ta louange arrive jusqu’aux extrémités de la terre. Ta droite est pleine de justice.
11 Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
Que la montagne de Sion se réjouisse, que les filles de Juda soient dans l’allégresse, à cause de tes jugements!
12 Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
Parcourez Sion et faites-en le tour, comptez ses forteresses;
13 mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
observez son rempart, examinez ses palais, pour le raconter à la génération future.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.
Voilà le Dieu qui est notre Dieu à jamais et toujours; il sera notre guide dans tous les siècles.