< Zaburi 48 >
1 Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
The song of salm, of the sones of Chore. The Lord is greet, and worthi to be preisid ful myche; in the citee of oure God, in the hooli hil of hym.
2 Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
It is foundid in the ful out ioiyng of al erthe; the hil of Syon; the sidis of the north, the citee of the greet kyng.
3 Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
God schal be knowun in the housis therof; whanne he schal take it.
4 Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
For lo! the kyngis of erthe weren gaderid togidere; thei camen into o place.
5 Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
Thei seynge so wondriden; thei weren disturblid, thei weren mouyd togidere, tremblyng took hem.
6 Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
There sorewis as of a womman trauelynge of child;
7 Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
in a greet spirit thou schalt al to-breke the schippis of Tharsis.
8 Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
As we herden, so we sien, in the citee of the Lord of vertues, in the citee of oure God; God hath foundid that citee with outen ende.
9 Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
God, we han resseyued thi mercy; in the myddis of thi temple.
10 Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
Aftir thi name, God, so thin heriyng is spred abrood in to the endis of erthe; thi riyt hond is ful of riytfulnesse.
11 Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
The hil of Sion be glad, and the douytris of Judee be fulli ioiful; for thi domes, Lord.
12 Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
Cumpasse ye Syon, and biclippe ye it; telle ye in the touris therof.
13 mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
Sette ye youre hertis in the vertu of him; and departe ye the housis of hym, that ye telle out in an other generacioun.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.
For this is God, oure God, in to withouten ende, and in to the world of world; he schal gouerne vs in to worldis.