< Zaburi 48 >

1 Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
Yahweh is great, and he deserves to be greatly praised in the city where he [lives], [which is built on Zion], his sacred hill.
2 Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
That city, on a high [hill], is beautiful; it is the city where the true [God], the great king, [lives], and it causes people all over the world to rejoice [when they see it].
3 Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
God is in the strong towers there, and he shows that he protects the people in that city.
4 Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
Many kings gathered [with their armies] to attack [that city],
5 Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
but when they saw it, they were amazed; they became terrified, and ran away.
6 Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
Because they were very afraid, they trembled like a woman who is about to give birth to a child;
7 Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
they shook [like] ships sailing from Tarshish are shaken by a strong wind.
8 Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
We had heard [that this city is glorious], and now we have seen that it is. It is the city in which Yahweh, the almighty one, [lives]. It is the city which God will preserve/protect forever.
9 Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
God, [here] in your temple we think about how you faithfully love us.
10 Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
You [MTY] are famous and (are praised/people praise you) all over the earth, because you rule powerfully [MTY] and justly.
11 Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
The people who live near Zion Hill should be happy! The people in [all] the cities [MTY] in Judah should rejoice because you judge people fairly.
12 Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
[You Israeli people should] walk around Zion [Hill] and count the towers there;
13 mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
notice the walls there and examine the forts in order that you can tell about them to your children.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.
[Say to them], “This is [the city that belongs to] our God, [the one who lives] forever; he will guide us all of our lives.”

< Zaburi 48 >