< Zaburi 48 >
1 Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
“A psalm of the sons of Korah.” Great is Jehovah, and greatly to be praised In the city of our God, upon his holy mountain.
2 Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
Beautiful in its elevation is Mount Zion, The joy of the whole earth; The joy of the farthest North is the city of the great king;
3 Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
In her palaces God is known as a refuge.
4 Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
For, lo! kings were assembled against it; They passed away together.
5 Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
As soon as they saw, they were astonished; They were confounded, and hasted away.
6 Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
There terror seized upon them, —Pain, as of a woman in travail;
7 Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
As when the east wind breaketh in pieces The ships of Tarshish.
8 Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
As we have heard, so have we seen In the city of the LORD of hosts, in the city of our God; God will establish it for ever. (Pause)
9 Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
We think of thy loving-kindness, O God! In the midst of thy temple!
10 Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
As thy name, O God! so thy praise, extendeth to the ends of the earth; Thy right hand is full of righteousness.
11 Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
Mount Zion rejoiceth, The daughters of Judah exult, On account of thy righteous judgments.
12 Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
Go round about Zion; number her towers;
13 mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
Mark well her bulwarks; count her palaces; That ye may tell it to the next generation!
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.
For this God is our God for ever and ever; He will be our guide unto death.