< Zaburi 48 >

1 Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
“A song and psalm by the sons of Korach.” Great is the Lord, and highly praised in the city of our God, [in] his holy mountain.
2 Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
A beautiful district, the joy of the whole earth, is mount Zion, the farthest north, the city of the great King.
3 Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
God is become known in her palaces as a defence.
4 Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
For, lo, the kings were assembled, they are passed away together.
5 Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
They indeed saw—[and] so they were astonished; they were terrified, they were confounded.
6 Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
Trembling seized on them there, pain, as on a woman in travail.
7 Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
With the east wind thou breakest the ships of Tharshish.
8 Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
As we have heard, so have we seen [it] in the city of the Lord of hosts, in the city of our God: God will establish it for ever. (Selah)
9 Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
We have reflected on thy kindness, O God, in the midst of thy temple.
10 Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
As thy name is, O God, so is thy praise over the ends of the earth: of righteousness is thy right hand full.
11 Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
Let mount Zion rejoice, let the daughters of Judah be glad, because of thy judgments.
12 Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
Compass Zion about, and walk round about her; number her towers.
13 mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
Direct your mind to her outer wall, mark carefully her palaces: in order that ye may tell it to the latest generation.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.
For this One is God, our God for ever and ever: he will be our guide even unto death.

< Zaburi 48 >