< Zaburi 48 >
1 Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
A Psalm of praise for the sons of Core on the second [day] of the week. Great is the Lord, and greatly to be praised in the city of our God, in his holy mountain.
2 Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
The city of the great King is well planted [on] the mountains of Sion, with the joy of the whole earth, [on] the sides of the north.
3 Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
God is known in her palaces, when he undertakes to help her.
4 Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
For, behold the kings of the earth were assembled, they came together.
5 Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
They saw, and so they wondered: they were troubled, they were moved.
6 Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
Trembling took hold on them: there were the pangs as of a woman in travail.
7 Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
You will break the ships of Tharsis with a vehement wind.
8 Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
As we have heard, so have we also seen, in the city of the Lord of hosts, in the city of our God: God has founded it for ever. (Pause)
9 Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
We have thought of your mercy, O God, in the midst of your people.
10 Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
According to your name, O God, so is also your praise to the ends of the earth: your right hand is full of righteousness.
11 Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
Let mount Sion rejoice, let the daughters of Judaea exult, because of your judgments, O Lord.
12 Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
Go round about Sion, and encompass her: tell you her towers.
13 mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
Mark you well her strength, and observe her palaces; that you may tell the next generation.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.
For this is our God for ever and ever: he will be our guide for evermore.