< Zaburi 48 >

1 Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
A Canticle Psalm. To the sons of Korah, on the second Sabbath. The Lord is great and exceedingly praiseworthy, in the city of our God, on his holy mountain.
2 Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
Mount Zion is being founded with the exultation of the whole earth, on the north side, the city of the great king.
3 Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
In her houses, God will be known, since he will support her.
4 Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
For behold, the kings of the earth have been gathered together; they have convened as one.
5 Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
Such did they see, and they were astonished: they were disturbed, they were moved.
6 Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
Trembling took hold of them. In that place, their pains were that of a woman in labor.
7 Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
With a vehement spirit, you will crush the ships of Tarshish.
8 Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
As we have heard, so we have seen, in the city of the Lord of hosts, in the city of our God. God has founded it in eternity.
9 Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
We have received your mercy, O God, in the midst of your temple.
10 Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
According to your name, O God, so does your praise reach to the ends of the earth. Your right hand is full of justice.
11 Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
Let mount Zion rejoice, and let the daughters of Judah exult, because of your judgments, O Lord.
12 Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
Encircle Zion and embrace her. Discourse in her towers.
13 mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
Set your hearts on her virtue. And distribute her houses, so that you may discourse of it in another generation.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.
For this is God, our God, in eternity and forever and ever. He will rule us forever.

< Zaburi 48 >