< Zaburi 47 >

1 Pigeni makofi, enyi watu wote; mpigieni Mungu kelele za ushindi.
למנצח לבני-קרח מזמור ב כל-העמים תקעו-כף הריעו לאלהים בקול רנה
2 Kwa maana Yahwe Aliye Juu anatisha; ni Mfalme mkuu dunia yote.
כי-יהוה עליון נורא מלך גדול על-כל-הארץ
3 Yeye anawatiisha chini yetu na mataifa chini ya miguu yetu.
ידבר עמים תחתינו ולאמים תחת רגלינו
4 Yeye huchagua urithi kwa ajili yetu, utukufu wa Yakobo ambaye alimpenda. Serah
יבחר-לנו את-נחלתנו את גאון יעקב אשר-אהב סלה
5 Mungu ameinuliwa juu kwa shangwe, Kwa mbiu ya shangwe Yahwe yu juu.
עלה אלהים בתרועה יהוה בקול שופר
6 Mwimbieni Mungu sifa, imbeni sifa; mwimbieni sifa Mfalme wetu, imbeni sifa.
זמרו אלהים זמרו זמרו למלכנו זמרו
7 Kwa maana Mungu ni Mfalme duniani kote; mwimbieni mkiwa na uelewa.
כי מלך כל-הארץ אלהים-- זמרו משכיל
8 Mungu anatawala mataifa yote; Mungu hukaa kwenye kiti cha enzi.
מלך אלהים על-גוים אלהים ישב על-כסא קדשו
9 Wakuu wa watu wamekusanyika pamoja kwa watu wa Mungu wa Ibrahimu; kwa kuwa ngao za duniani ni za Mungu; yeye ameinuliwa juu sana.
נדיבי עמים נאספו-- עם אלהי אברהם כי לאלהים מגני-ארץ-- מאד נעלה

< Zaburi 47 >