< Zaburi 46 >

1 Mungu kwetu ni kimbilio la usalama na nguvu, upatikanao tele wakati wa mateso.
In finem, filiis Core, pro arcanis. Psalmus. Deus noster refugium et virtus; adjutor in tribulationibus quæ invenerunt nos nimis.
2 Hivyo hatutaogopa, hata kama dunia italazimika kubadilika, hata kama milima italazimika kutetemeka na kuangukia kwenye mtima wa bahari, hata kama maji yatavuma kwa kishindo kikuu,
Propterea non timebimus dum turbabitur terra, et transferentur montes in cor maris.
3 hata kama milima itatetemeka kwa vurugu ya maji. (Selah)
Sonuerunt, et turbatæ sunt aquæ eorum; conturbati sunt montes in fortitudine ejus.
4 Kuna mto, mikondo yake huufanya mji wa Mungu kufurahi, mahali patakatifu pa hema ya Aliye Juu.
Fluminis impetus lætificat civitatem Dei: sanctificavit tabernaculum suum Altissimus.
5 Mungu yuko katikati yake; naye hatasogezwa; Mungu atamsaidia, naye atafanya hivyo asubuhi na mapema.
Deus in medio ejus, non commovebitur; adjuvabit eam Deus mane diluculo.
6 Mataifa yalikasirika na falme zikataharuki; yeye alipaza sauti yake, na nchi ikayeyuka.
Conturbatæ sunt gentes, et inclinata sunt regna: dedit vocem suam, mota est terra.
7 Yahwe wa majeshi yuko pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu la usalama. (Selah)
Dominus virtutum nobiscum; susceptor noster Deus Jacob.
8 Njoni, mtazame matendo ya Yahwe, uharibifu alioufanya juu ya nchi.
Venite, et videte opera Domini, quæ posuit prodigia super terram,
9 Anaisitisha vita kwenye nchi; yeye anauvunja upinde na kuikata vipande vipande mishale; anazichoma ngao.
auferens bella usque ad finem terræ. Arcum conteret, et confringet arma, et scuta comburet igni.
10 Mkae kimya na mjue kuwa mimi ni Mungu; nitainuliwa juu ya nchi.
Vacate, et videte quoniam ego sum Deus; exaltabor in gentibus, et exaltabor in terra.
11 Mungu wa majeshi yuko pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu la usalama. Serah
Dominus virtutum nobiscum; susceptor noster Deus Jacob.

< Zaburi 46 >