< Zaburi 46 >
1 Mungu kwetu ni kimbilio la usalama na nguvu, upatikanao tele wakati wa mateso.
Al maestro del coro. Dei figli di Core. Su «Le vergini...». Canto. Dio è per noi rifugio e forza, aiuto sempre vicino nelle angosce.
2 Hivyo hatutaogopa, hata kama dunia italazimika kubadilika, hata kama milima italazimika kutetemeka na kuangukia kwenye mtima wa bahari, hata kama maji yatavuma kwa kishindo kikuu,
Perciò non temiamo se trema la terra, se crollano i monti nel fondo del mare.
3 hata kama milima itatetemeka kwa vurugu ya maji. (Selah)
Fremano, si gonfino le sue acque, tremino i monti per i suoi flutti.
4 Kuna mto, mikondo yake huufanya mji wa Mungu kufurahi, mahali patakatifu pa hema ya Aliye Juu.
Un fiume e i suoi ruscelli rallegrano la città di Dio, la santa dimora dell'Altissimo.
5 Mungu yuko katikati yake; naye hatasogezwa; Mungu atamsaidia, naye atafanya hivyo asubuhi na mapema.
Dio sta in essa: non potrà vacillare; la soccorrerà Dio, prima del mattino.
6 Mataifa yalikasirika na falme zikataharuki; yeye alipaza sauti yake, na nchi ikayeyuka.
Fremettero le genti, i regni si scossero; egli tuonò, si sgretolò la terra.
7 Yahwe wa majeshi yuko pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu la usalama. (Selah)
Il Signore degli eserciti è con noi, nostro rifugio è il Dio di Giacobbe.
8 Njoni, mtazame matendo ya Yahwe, uharibifu alioufanya juu ya nchi.
Venite, vedete le opere del Signore, egli ha fatto portenti sulla terra.
9 Anaisitisha vita kwenye nchi; yeye anauvunja upinde na kuikata vipande vipande mishale; anazichoma ngao.
Farà cessare le guerre sino ai confini della terra, romperà gli archi e spezzerà le lance, brucerà con il fuoco gli scudi.
10 Mkae kimya na mjue kuwa mimi ni Mungu; nitainuliwa juu ya nchi.
Fermatevi e sappiate che io sono Dio, eccelso tra le genti, eccelso sulla terra.
11 Mungu wa majeshi yuko pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu la usalama. Serah
Il Signore degli eserciti è con noi, nostro rifugio è il Dio di Giacobbe.