< Zaburi 46 >

1 Mungu kwetu ni kimbilio la usalama na nguvu, upatikanao tele wakati wa mateso.
TO THE OVERSEER. BY SONS OF KORAH. FOR GIRLS’ [VOICES]. A SONG. God [is] our refuge and strength, A most sure help in adversities.
2 Hivyo hatutaogopa, hata kama dunia italazimika kubadilika, hata kama milima italazimika kutetemeka na kuangukia kwenye mtima wa bahari, hata kama maji yatavuma kwa kishindo kikuu,
Therefore we do not fear in the changing of earth, And in the slipping of mountains Into the heart of the seas.
3 hata kama milima itatetemeka kwa vurugu ya maji. (Selah)
Roar—troubled are its waters, Mountains shake in its pride. (Selah)
4 Kuna mto, mikondo yake huufanya mji wa Mungu kufurahi, mahali patakatifu pa hema ya Aliye Juu.
A river—its streams make glad the city of God, Your holy place of the dwelling places of the Most High.
5 Mungu yuko katikati yake; naye hatasogezwa; Mungu atamsaidia, naye atafanya hivyo asubuhi na mapema.
God [is] in her midst—she is not moved, God helps her at the turn of the morning!
6 Mataifa yalikasirika na falme zikataharuki; yeye alipaza sauti yake, na nchi ikayeyuka.
Nations have been troubled, Kingdoms have been moved, He has given forth with His voice—earth melts.
7 Yahwe wa majeshi yuko pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu la usalama. (Selah)
YHWH of Hosts [is] with us, The God of Jacob [is] a tower for us. (Selah)
8 Njoni, mtazame matendo ya Yahwe, uharibifu alioufanya juu ya nchi.
Come, see the works of YHWH, Who has done astonishing things in the earth,
9 Anaisitisha vita kwenye nchi; yeye anauvunja upinde na kuikata vipande vipande mishale; anazichoma ngao.
Causing wars to cease, To the end of the earth, He shatters the bow, And He has cut apart the spear, He burns chariots with fire.
10 Mkae kimya na mjue kuwa mimi ni Mungu; nitainuliwa juu ya nchi.
Desist, and know that I [am] God, I am exalted among nations, I am exalted in the earth.
11 Mungu wa majeshi yuko pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu la usalama. Serah
YHWH of hosts [is] with us, The God of Jacob [is] a tower for us! (Selah)

< Zaburi 46 >