< Zaburi 45 >

1 Moyo wangu unafurika kwa neno zuri; nitasoma kwa sauti maneno niliyo yaandika kuhusu mfalme; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mwenye ustadi.
Unto the end. For those who will be changed. To the sons of Korah, toward understanding. A Canticle for the Beloved. My heart has uttered a good word. I speak of my works to the king. My tongue is like the pen of a scribe who writes quickly.
2 Wewe u mzuri sana kuliko mwanadamu yeyote; neema imemiminwa midomoni mwako; Kwa hiyo tunajua ya kuwa Mungu amekubariki milele.
You are a brilliant form before the sons of men. Grace has been poured freely into your lips. Because of this, God has blessed you in eternity.
3 Weka upanga wako upande wako, wewe uliye mwenye nguvu, katika utukufu wako na enzi yako.
Fasten your sword to your thigh, O most powerful one.
4 Katika enzi yako enenda katika ushindi kwa sababu ya uaminifu, upole, na haki; mkono wako wa kuume utakufundisha mambo ya kutisha.
With your splendor and your excellence extended, proceed prosperously, and reign for the sake of truth and meekness and justice, and so will your right hand lead you wondrously.
5 Mishale yako ni mkali; watu huanguka chini yako; mishale yako imo ndani ya mioyo ya adui za mfalme.
Your arrows are sharp; the people will fall under you, with the hearts of the enemies of the king.
6 Kiti chako cha enzi, Mungu ni cha milele na milele; na fimbo ya haki ni fimbo ya utawala wako.
Your throne, O God, is forever and ever. The scepter of your kingdom is a scepter of true aim.
7 Umeipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekupaka mafuta ya furaha kuliko wenzako.
You have loved justice and hated iniquity. Because of this, God, your God, has anointed you, before your co-heirs, with the oil of gladness.
8 Mavazi yako yote hunukia manemane, udi, na mdalasini; kukoka katika majumba ya pembe vyombo vya muziki wa nyuzi vimekufurahisha.
Myrrh and balsam and cinnamon perfume your garments, from the houses of ivory. From these, they have delighted you:
9 Binti za wafalme ni kati ya wake zako waheshimiwa; na mkono wako wa kuume amesimama malikia aliye vaa mavazi ya dhahabu ya Ofiri.
the daughters of kings in your honor. The queen assisted at your right hand, in clothing of gold, encircled with diversity.
10 Sikiliza, mwanangu, tafakari na utege sikio lako; uwasahahu watu wako na watu wa nyumba ya baba yako.
Listen, daughter, and see, and incline your ear. And forget your people and your father’s house.
11 Hivyo mfalme atautamani uzuri wako; yeye ni Bwana wako; umstahi.
And the king will desire your beauty. For he is the Lord your God, and they will adore him.
12 Binti wa Tiro atakuwepo akiwa na zawadi; matajiri kati wa watu watajipendekeza kwako.
And the daughters of Tyre will entreat your countenance with gifts: all the rich men of the people.
13 Binti mfalme katika jumba la kifahari ana utukufu wote; mavazi yake yametengenezwa kwa dhahabu.
All the glory of the daughter of its king is inside, in golden fringes,
14 Naye ataongozwa kwa mfalme akiwa katika mavazi ya dhahabu; mabikra, wenzake wanoumfuata, wataletwa kwako mafalme.
clothed all around with diversities. After her, virgins will be led to the king. Her neighbors will be brought to you.
15 Wao wataongozwa kwa furaha na shangwe; wataingia mahali pa mfalme.
They will be brought with gladness and exultation. They will be led into the temple of the king.
16 Katika mahali pa baba zako watoto wako watakuwepo, ambao wewe utawafanya kuwa wakuu katika nchi yote.
For your fathers, sons have been born to you. You will establish them as leaders over all the earth.
17 Nami nitalifanya jina lako kukumbukwa katika uzao wote; kwa hiyo watu watakushukuru milele na milele.
They will remember your name always, for generation after generation. Because of this, people will confess to you in eternity, even forever and ever.

< Zaburi 45 >